MWENYEKITI wa Baraza la Wazee wa Chama
cha Demokrasia na Maendeleo Taifa, (Chadema),
Hashim Juma Issa, amesema kuwa serikali ya Baraza la Mapinduzi Zanzibar ni ‘feki’.
Mwenyekiti huyo, amabaye alikuwa mgeni
rasmi, alitoa kauli hiyo wakati wa Kongamano la Baraza la Wazee wote wa Chadema
wanaoishi katika jimbo la Ukonga jijini Dar
es Salaam juzi.
Alisema, hivyo, kwa vile kuna ushahidi unaoonesha
kuwa Wazanzibari wote ni Watanzania kutokana na kuwa na vipande vya uraia wa Tanzania ambapo Rais wake ni Jakaya Kikwete, kitendo hicho kitendo
kinadhirisha wazi kuwa Zanzibar
haina raia wala serikali yake.
“Ndugu zangu mimi ni mzanzibari tutaitetea
Zanzibar kwa
nguvu zetu zote simuogopi mtu yeyote muda wa kuogopana umekwisha iliyobaki sasa
ni vitendo,”alisema Juma.
Juma, alisema anashangaa kumuona Dk. Muhamed
Ali Shein kujidai kuwa ni Rais wa Zanzibar
wakati hakuna raia hata mmoja Wazanzibar kwa hiyo alimtaka rais huyo aeleze
raia wakwe wako wapi.
“Sasa huna huruma, kama huna raia wewe ni
rais wa nani, ile iliyoko Zanzibar
ni Serikali feki, Wazanzibari watambue kuwa hawana serikali hawa wanajidanganya,”alisema.
Juma, alisema Tanzania kuna serikali moja wasiwadanganye
wananchi, kutokana na mazingira hayo Chadema inataka kuleta mfumo wa serikali
tatu, ambazo zitakuwa ni Tanganyika,
Zanzibar zote
hizo kila moja ikiwa na mamlaka yake.
Alisema, baada ya kuanzishwa serikali
hizo kutakuwa na serikali moja ya shirikishoku hivyo kuwa taka wazee kusimamia hilo kwa kutumia hekima zenu.
Kuhusu Wazee, Mwenyekiti huyo, aliwaomba
wazee hao wapinge baadhi ya maneno ya wanasiasa kuwa Chadema hivi sasa hakina
uwezo wa kutongoza kwa maana ya kutoa rais wa nchi bali hadi mwaka 2020.
Aliema kuanzia sasa wazee watambue kuwa
wana jukumu kubwa alikutoa ushauri ambao utakisaidia chama wakati kikielekea
kipindi cha Uchaguzi Mkuu.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo, Suzan Lymo, alisema
kuwa Sera ya Chadema iko wazi kuhusu wazee, kwani kitakapoingia madarakani
kitakuwa na utaratibu wa kuwalipa pensheni.
Alisema utaratibu wa serikali ya sasa
umekuwa ukibagua katika kuwalipa pensheni wazee kwani wanaolipwa ni wale
walikuwa wakifanya kazi katika za umma.
Aidha, aliwataka wazee kuhamasishana
katika suaala la kujiandikisha katika daftari la mpiga kura kwa vile bila ya
kufanya hivyo watakosa fursa ya kupiga kura Oktoba mwaka huu.
“Nawaomba wazee kuanzia sasa msikae
kimya huu uwe ni mwanzo mzuri, muwe mnatoa matamko pindi mnapoona mambo
yanaharibika hukuchi,’alisema.
Susan, aliongeza kuwa pia wazee hao
watumie hekima zao kwa kujiepusha kwa kujiingiza katika migogoro hususan kwa
kuwapendelea baadhi ya wanachama wanaotaka kugombea nafasi za uongozi.
No comments:
Post a Comment