KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Wednesday, 13 May 2015

DK. LUMBANGA AWASHUKIA WANALALAMIKIA SHERIA YA PPRA



MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Manunuziya Umma (PPRA), Dk. Matern Lumbanga, ameshangazwa na baadhi ya mawaziri wanaosema kuwa Sheria ya manunuzi ni mbaya wakati wameipitisha wenyewe bungeni.
Ikumbukwe manunuzi ya umma huchukua takriban nusu ya fedha za bajeti yote ya serikali, hivyo usimamizi mzuri katika sekta hiyo unahitaji mchngo wa wadau wote ili kuhakikisha upatikanaji wa thamani bora ya fedha za umma.
Kauli hiyo aliitoa jijini Dar es Salaama jana wakati alipozungumza na wandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya PPRA kutimiza miaka 10 tangu ilipoanzishwa mwaka 2005.
Dk. Lumbanga, alisema wote wanaolalamikia Sheria hiyo na kudai kuwa ni mbaya, inatikana sheria hiyo kuwanyima kufanya vitendo vyao vya kifisadi katika fedha za umma.
Aliongeza kwa kusema kuwa kuna baadhi ya idara za serikali zimekuwa zikienda kinyume na sheria hiyo, kwa kutoa zabuni bila ya kuzitangaza.
“Kazi ya Sheria hiyo ni kusimamia na kudhibiti manunuzi ya umma yasiweze kutumika kinyume na sheria,”alisema Dk. Lumbanga.
Alisema, serikali ikifanikiwa kudhibiti manunuzi nje ya sheria hiyo, basin chi kupiga hatua kimaendeleo na kupunguza umasikini.
Aidha, alisema inapobainika kunawaliofanya manunuzi kinyume cha sheria hiyo, PPRA haiwaachi na kwamba inawachukulia hatua za kisheria.
Akizungumzia maadhimisho hayo, Dk Lumbanga, alisema yatafanyika siku tatu kuanzia Mei 18 hadi 21 mwaka huu ambapo yatazinduliwa na Waziri waziri wa Fedha na Uchumi Saada Mkuya, atayazindua Mei 19 mwaka huu, yatafanyika katika ukumbi wa Dimond Jubilee.
Alisema, lengo maadhimisho hayo ni kuwakutanisha wadau wa manunuzi ya umma nchini kujadili mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya hiyo muhimu hususan katika kipindi hicho cha muongo mmoja wa uwepo wa mfumo imara wa usimamizi na udhibiti  manunuzi.
Aidha, wadau watapata fursa ya kujadili matatizo mbalimbali ambayo wanakabiliana nayo katika sekta hiyo na kupendekeza mikakati yenye lengo la kuboresha zaidi.
Dk. Lumbanga alisema maadhimisho hayo yataanza kwa wasrsha maalum ya wadau wa habari hususan wandishi habari kutoka mikoa mikoa yote nchini, wahariri, wakilishi kutoka Baraza la Habari Tanzania (MCT) na Umoja wa klabu za waandishi wa habari Tanzania (UTPC).
“Warsha hiyo itafanyika Mei 18 mwaka huu katika ukumbi wa Diamond Jubilee,”alisema Dk. Lumbanga.
Dk. Lumbanga, ametoa wito kwa wadau wote wa manunuzi nchini na umma kwa ujumla kujitokeza kushiriki kwenye maadhimisho hayo.


No comments:

Post a Comment