KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Wednesday, 13 May 2015

KAMANDA MPINGA: MAFUNZO KWA MADEREVA YASITISHWA



KIKOSI cha Usalama Barabarani nchini, kimetangaza   rasmi kutokuepo kwa mafunzo ya madereva wote wanaoendesha vyombo vya moto wala kutakiwa kwenda kusoma kwa mwaka huu.
Hivi  karibuni  serikali ilipitisha sheria  ya barabarani ya mwaka 1977 ambayo  iliboreshwa, ikiwataka  madereva  kwenda kusoma pamoja na gharama ya mafunzo kutakiwa kulipa ada ya  sh.560,000.
Sheria hiyo pia iliwataka  madereva wa magari mengine kuchunguzwa afya zao na kujaribiwa kila baada ya miaka sita.(The Road Traffic Examination ana Re-Testing of Drivers)  Regulation GN No 31 ya januari 30 mwaka huu.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamanda  wa kikosi hicho, Mohammed Mpinga, alisema Sheria hiyo ilisababisha madereva hao kugoma kusafirisha  abiria na mizigo hali iliyosababisha adha kubwa kwa wananchi pamoja na kuathiri uchumi wanchi.
Mpinga, alisema hayo kwa vile mitaala ya mafunzo hayo mafupi haijakamilika na shule zitakazohusika hazijaanishwa pia  ada za mafunzo hazijapangwa.
Alisema,  kuwa  ada ya sh 560,000 iliyotangazwa hivi karibuni haijawahi kutamkwa na serikali bali ilitamkwa kienyeji na Mkuu wa chuo cha Taifa cha usafirishaji(NIT), Dk. Zakaria Mganilwa.
Mpinga, lisema serikali imesitisha sheria ya kwenda kusoma kwa mwaka huu na kudai kuwa  itakamilishwa mwaka ujao wa bajeti 2016 hadi 2017 ambapo mpaka kufikia  hapo madai ya madereva hao watakuwa wamekamilishwa na kuboreshewa.
Aliongeza kuwa  kwa madereva ambao leseni zao zimekwisha au zitaisha katika kipindi hiki watabadilishiwa na kuhusisha leseni zao kwa utaratibu wa zamani bila kuulizwa vyeti vya mafunzo mafupi (Refresher course).na kuwataka watakao ulizwa watoe taarifa.
“Nawataka madereva wote wawe na uvumilivu kwa matatizona changamoto zao kwani kamati ya Kudumu ya kutatua matatizo katika sekta ya usafirishaji iliyoundwa na waziri mkuu itayapatia ufumbuzi wa kudumu”alisema Mpinga.
Kwa upande wake mwenyekiti wa madereva nchini, Clement Masanja, alisema Kamati iliyoundwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda,  ilipewa taarifa kuwa sheria ya kuwataka madereva kwenda kusoma mwaka huu imefutwa.
“Kuanzia sasa hakuna dereva atakayeulizwa habari ya cheti, imeundwa tume ambayo imeshaanza  kazi hakuna kusoma ila madereva wafuate sheria za barabarani, nawatakia madereva wote wafanye kazi kwa amani  na utulivu kwani haki zao zimeanza kuboreshwa.”alisema
Masanja.

No comments:

Post a Comment