KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday, 12 May 2015

MKAPA MGENI RASMI KATIKA MKUTANO WA WAWAKANDARASI MEI 14

RAIS Mstaafu Benjamini Mkapa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Mkutano wa Bodi ya Wakandarasi unaotarajiwa kufanyika Mei 14 hadi 15 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Akitoa taarifa hiyo katika Ofisi ya Bodi ya Usajili wa Wahandisi, Mwenyekiti wa Maandalizi ya Bodi hiyo Mhandisi Dk Mwakyusa Ambwene, alisema kwa kawaida mkutano huo utawahusisha wadau wote wa sekta ya ujenzi.
Alisema siku hiyo kutakuwa na shughuli mbalimbali zitakazoanywa ikiwa ni pamoja na majadiliano ya kitaaluma, kiapo cha wahandisi wataalamu.
Dk. alisema pia kutakuwa na maonyesho mbalimbali ya kiufundi na biashara vifaa vinavyohusiana na ujenzi.
Naye, Msajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB), Jehad Abdallah Jehad, amezitaka Taasisi, Mashirika na wafanyabiashara mbalimbali kutumia fursa hiyo kuonyesha bidhaa zao katika mkutano huo wa mbili ili kudhihirishia umma juu ya kazi wanazozifanya kwa maendeleo ya nchi.
Aliongeza kuwa mkutano huo una lengo la kuwatia moyo wanafunzi wa kitanzania wanaosomea uhandisi ili wafanye vizuri zaidi katika masomo yao na kuwafanya vijana washawishike kusomea taaluma hiyo.

No comments:

Post a Comment