KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday, 10 May 2015

ELIZABETH MISSOKIA, ANG'ATUKA UKURUGENZI MTENDAJI HakiELIMU

Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu aliyemaliza muda wake Elizabeth
SHIRIKA la HakiElimu litaendeleza harakati zake za kuwapatia taarifa mbalimbali  wananchi ili waweze kushiriki katika kuchangia mwazo ambayo yatasaidia kuboresha elimu na demokrasia kuanzia ngazi ya kitongoji hadi Taifa.

John Kalage (JK), alitoa kauli hiyo wakati wa hafla fupi ya kumuaga Elizabeth Missokia ambaye alikuwa  Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo kwa pindi cha miaka saba na kumkaribisha mkurugenzi mpya ambaye ni Kalage.
 Kalage, alisema hivyo kwa vile bila ushiriki wa wananchi HakiElimu pekee yake haiwezi kutekeleza malengo yake ambayo yanalenga kufikia usawa, ubora, haki na demokrasia katika utoaji wa elimu katika jamii.
Mkurugenzi huyo mpya, alisema kuwa anaamini elimu bora inasidia, inakuza usawa, ubunifu, udadisi, na demokrasia kwa ujumla. 
“Harakati za wadau wa elimu ni mojawapo ya nyenzo zinazotumika kuhamasisha  ushiriki huu wa wananchi na hizi ni harakati za wananchi, mashirika na  taasisi zenye nia ya kuongeza kasi ya kuleta mabadiliko chanya katika elimu  na demokrasia nchini,”alisema JK.Aidha, Kalage ameahidi kutekeleza kwa vitendo yale yote yaliyoanzishwa na mtangulizi wake ikiwemo kuanzishwa shule itakayo kuwa mfano wa elimu bora, inayotakiwa kutolewa katika shule zote nchini.
Elizabeth, wakati akiwaaga wafanyakazi wenzake, alisema kufanya kazi katika shirika hilo kunataka wakati mwingine kuwa na kichwa cha mwendawazimu.Alisema hivyo kutokana na baadhi ya watendaji waserikali kulichukulia shirika hilo kama vile linawapotosha wananchi kuhusu atua mbalimbali zinazotekelezwaa na serikali.
“Shirika halina nia mbaya na linaamini yapo mengi mazuri yaliyofanywa na kila wanachokikosoa lengo lake ni kuwatakiwa watoto wa wote wa Tanzania wapate elimu ambayo itawaokoa ‘na ufaulu wa ‘zero’,”alisema Elizabeth.Elizabeth, aliwaasa wafanyakazi wezake waliobaki kuwa wasikate tamaa bali waongeze kasi katika mapambano yao ya kuleta mapinduzi yatakayosaidia watoto wa kitanzania kupata elimu bora na siyo bora elimu.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Utekelezaji cha Miradi ya Matokeo Makubwa sasa (BRN), kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Grace Hoka, alisema serikali inatambua kazi nzuri ya shirika hilo na iko tayari kushirikiana nalo kinyume na baadhi ya wadau wanavyo dhani.

No comments:

Post a Comment