KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday, 10 May 2015

TAWLA YATIMIZA MIAKA 25 TANGU KUANZISHWA



Badhi ya Watendaji wa TAWLA wakiwa na Mkurugenzi Mtendaji, Tike Mwambipile, aliyevaa kofia 

ZAIDI ya watu milioni 15 wenye matatizo ya kisheria wamepata msaada wa huo kupitia Chama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA), tangu kilipoanzishwa miaka 25 iliyopita.
Hayo yalisemwa leo, Mkurugenzi Mtendaji wa TAWLA, Tike Mwambipile wakati alipozungumza na wandishi wa habari kuhusu ratiba ya maadhimisho ya sherehe za chama hicho, kutimiza miaka hiyo, ambapo pia watatoa elipmu kuhusu masuala ya sheria.
Alisema pamoja na kutoa msaada huo wa kisheria, pia wameweza kuihamasisha jamii juu ya masuala ya kisheria kupitia machapisho mbalimbali, mafunzo kwa wasaidizi wa kisheria.
“Pia tumeweza kuwafikia kwa kupitia vyombo vya habari, michezo ya kuigiza vyote hivyo vivilikuwa vichocheo ambavyo vimetufanya tuwafikie watu hao milioni 15,”alisema Tike.
Akizungumzia ratiba ya sherehe hizo, alisema kuwa zilianza jana hadi Mei 30 kutakuwa na mwendelezo wa vipindi vya kuelimisha jamii kuhusu masuala ya sheria na haki za binadamu kupitia vyombo vya habari katika mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma,Tanga na Arusha.
Aliongeza kuwa katika maadhimisho hayo Mei 29 mwaka huu kutakuwa na matembezi kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu hadi Karimjee na kupokelewa na Rais Jakaya Kikwete.
Tike alisema siku inayofuata kutakuwa na Mkutano Mkuu wa wanachama na jioni ambao utazungumzia mizungumzia mipango ya baadae ikiwa ni jinsi gani chama hicho kitafanyakazi katika mikoa yote nchini.

No comments:

Post a Comment