Kata hiyo, hivi sasa inashikiliwa
na Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (Chadema).
Hata hivyo, ili apate
nafasi hiyo atahitaji kwanza ridhaa ya
chama chake baada ya kufanyika kura za ndani.Akizungumza na mwandishi wa Sauti
Pevu jijini juzi, Kyaruzi, alisema, akifanikiwa katika harakati zake hizo anatarajia
kutumia sera zake ujana zaidi.
“Sera zangu ni tofauti kwa
vile naamini diwani aliyopo ametekeleza ahadi zake kwa sehemu yake hivyo,
ninachotaka ni kumpokea, ukichukulia kuwa mimi ni kijana nataka kutumia sera
zangu za ujana,”alisema Kyaruzi.
Alisema msukumo wa kugombea
nafasi hiyo umetokana na kubaini kwake matatizo yanayowakabili wakazi wa kata
hiyo.
Aliyataja, matatizo hayo
kuwa ni eneo hilo
kugeuzwa kuwa kambi ya watumiaji wa dawa za kulevya (Mateja), uchafu
uliyokithiri na vijana kutopenda kufanyakazi.
Aidha, ili yote hayo
yafanikiwe, anapaswa kujenga umoja na ushirikiano kitu ambacho hivi sasa
kinakosekana katika kata hiyo.
“Kwa Kata ya Kimanga
nasubiri tu uwamuzi wa ndani wa chama changu lakini kwa upande wa wakazi
wenzangu wananiamini bila shaka najiamnini kwa hilo,”alisema Kyaruzi.
MWISHO
No comments:
Post a Comment