HALMASHAURI ya Manispaa ya Kisarawe, mkoani Pwani imetangaza viwanja 291 kwa ajili ya fursa za uwekezaji kwa wawekezaji wa ndani na nje kuanzia sasa.
Fursa hiyo inakuja baada ya wilaya hiyo kuanzisha Mradi wa Uendelezaji wa Ardhi, Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kisarawe katika kipindi cha mwaka 2013/14.
Akizungumza na waandishi wa habari jana wilayani hapa, Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Mwanvua Mrindoko, alisema viwanja hivyo viko katika maeneo ambayo hayana migogoro.
Mrindoko alisema eneo hilo ambalo linafaa kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda linapatikana katika Kijiji cha Visegese, kilomita nne kutoka mji mdogo wa Kisarawe.
“Katika eneo hili kuna njia mbili za reli ambazo zinapita karibu kabisa na eneo hili la uwekezaji, pia haliko mbali na Barabara ya Morogoro.
“Nawaomba kila anayehitaji kuwekeza anakaribishwa Kisarawe kwani fursa zote ikiwemo ubora wa miondombinu vinapatikana kirahisi,” alisema Mrindoko.
Naye Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Adam Ng’imba, aliwatahadharisha wananchi na kuwataka watambue kuwa ardhi isiyopimwa na kumilikishwa inakosa thamani halisi na kushindwa kumtajirisha mmiliki wake.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kisarawe Bi Mwananvua Mrindoko akizungumza katika mkutano huo kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, Katikati Ng’imba Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kisarawe na kushoto ni Cheyo Kelege Afisa Ardhi na Maliasili Kisarawe.
Katikati ni Adam Ng’imba Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kisarawe na kushoto ni Cheyo Kelege Afisa Ardhi na Maliasili Kisarawe na kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kisarawe Mwananvua Mrindoko wakizungumza na wanahabari kuhusu mradi huo.
Mkutano huo ukiendelea
Kitabu kinachouelezea mradi huo
No comments:
Post a Comment