MWANDISHI wa mtandao huu Alphonce Tonny Kapelah kutoka Mtwara ameona aufahamishe umma juu ya mwasisi wa jina la Tanzania.
Mwandishi aliandika makala haya
wakati ilipotimiaka 50 ya Uhuru wa Tangayika, najua wengi wetu hatujui historia
ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar maana tuliwakuta waasisi wetu
wameishafanya zoezi hilo,tusilijadili sana
kwa kuwa lengo lao lilikuwa zuri.
Lakini je unamjua huyu Bwana
aliyetunga jina la Tanzania pata historia ya namna alivyofanikiwa kupata jina la T
A N Z A N I A
Sherehe za Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar
huwa tunasherekea kila Mwaka Tarehe 26/04/ lakini Tangu mimi binafsi nipate
ufahamu na kuanza kushuhudia sherehe za Muungano nimekuwa nikisikia kuwa jina
la Tanzania lilipendekezwa
na Watanganyika, Wazanzibar na Raia wengine wa nje lakini sikuwahi kukutana na
huyo ambae alibuni jina hili tamu la Tanzania.
Imekuwa kama Bahati nimekutana na
Mtu huyu aliyebuni jina la Tanzania Mkoani Mtwara,sehemu ambayo tayari naiweka
kwenye Historia yangu hata kesho nikiondoka Mtwara nitaikumbuka Radio
yangu Safari Radio.
Huyu bwana aliyebuni jina la Tanzania ni Muhindi na Dini yake ni AHMADIYA
MUSLIM JAMAAT TANZANIA
majina yake ni MOHAMMED IQBAL DAR.
Mohammed alizaliwa Mkoani Tanga miaka ya 1944,Baba mzazi wa
Mohammed alikuwa Daktari huko mkoani Morogoro alikuwa anaitwa Dr. T A
DAR alikuwa Tanganyika
kuanzia mwaka 1930.
Mohammed Iqbal Dar alipata elimu
yake ya Msingi Mkoani Morogoro shule ya Msingi H H D AGAKAN kwa sasa ni Shule
ya Serikali na baada ya Hapo alikuja baadae kujiunga na Chuo cha Mzumbe akasoma Kidato cha Kwanza mpaka cha Sita.
Aliingiaje kwenye shindano la
kupendekeza jina la Muungano kati Tanganyika na Zanzibar,Mohammed anasema
alikuwa Maktaba akijisoma gazeti la Tanganyika Standard siku hizi Daily News
akaona Tangazo linasema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unafahamika kama
Republic of Tanganyika and Zanzibar jina likaonekana refu sana kwa hiyo
Wananchi wote wakaombwa Washiriki kwenye shindano la Kupendekeza jina moja litakalo
zitaja nchi zote mbili yaani Tanganyika na Zanzibar
Mohammed Iqbal Dar anasema
aliamua kuingia kwenye Shindano na hivi ndivyo alianza Safari ya Kubuni Jina la
Muungano,Kwanza anasema alichukua karatasi akaandika Bismillah Raahman Rahimu
hii ni kutokana na Imani yake na baada ya hapo akaandika jina la Tanganyika
baada ya hapo akaandika Zanzibar halafu akaandika jina lake Iqbal halafu
akaandika jina la Jumuiya yake ya Ahmadiya baada ya Hapo akamrudia tena
Mwenyezi Mungu akamwomba amsaidie ili apate jina zuri kutoka katika majina hayo
aliyokuwa ameyaandika.
Baada ya hapo Mohammed Iqbal Dar
alichukua herufi tatu kutoka Tanganyika yaani TAN na kwa upande wa Zanzibar
akachukua Herufi tatu za Mwanzo ZAN ukiunganisha unapata TANZAN alivyoona hivyo
akachukua I herufi ya kwanza katika jina lake la Iqbal na akachukua A kutoka jina
la dini yake yaani Ahmadiyya kwa maana hiyo ukiongeza herufi hizi mbili I na A
kwenye TANZAN unapata jina kamili TANZANIA akalisoma jina akaliona ni zuri
lakini akajiridhisha pia kwamba akiongeza herufi hizo za I na A kwenye TANZAN
italeta maana kwakuwa nchi nyingi za Afrika zinaishia na IA.
mfano
EthiopIA,ZambIA,NigerIA,TunisIA,SomalIA,GambIA,NamibIA,LiberIA,MauritanIA
alivyoona hivyo akaamua apendekeze kuwa jina TANZANIA ndio litumike kuwakilisha
nnchi hizi mbili yaani Tanganyika na Zanzibar kwa maana hiyo jina TANZANIA
limezaliwa kutoka majina manne majina hayo ni Tanganyika,Zanzibar,Iqbal na
Ahmadiyya
Mohammed Iqbal Dar baada ya
kupata jina hilo akalituma jina hilo kwenye kamati ya kuratibu
Shindano
Baada ya Muda mwingi kupita
baba yake na Mohammed Iqbal Dar alipokea Barua nzito kutoka serikalini ikiwa
inasomeka kama ifuatavyo…
No comments:
Post a Comment