SHIRIKA LA UMEME
TANZANIA
(TANESCO)

TAARIFA YA KUREJEA KATIKA HALI YA KAWAIDA KWA
HUDUMA YA LUKU
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kuwataarifu
wateja wake wote wanaonunua umeme wa LUKU kwa njia ya mitandao kwamba, huduma
hiyo kwa sasa imerejea kwenye hali ya kawaida.
Itakumbukwa kwamba kulitokea usumbufu kwa wateja wetu
kushindwa kununua umeme wa LUKU baada ya TANESCO kusitisha huduma kwa mmoja wa
Mawakala wake Aprili 28, 2015.
Tunapenda kuwahakikishia na kuwaondoa hofu wateja wetu wote
kwamba mfumo wa LUKU wa Tanesco upo salama na waendelee kununua umeme kupitia
mitandao na mawakala wetu kama kawaida.
Shirika linawaomba wateja wote wenye matatizo ya kutopata
“Units” baada ya kutuma pesa zao au “Units” kushindwa kuingia kwenye mita, wawasiliane
na Ofisi yoyote ya Tanesco iliyokaribu.
Uongozi wa Shirika unaomba radhi kwa usumbufu wowote
uliojitokeza katika kipindi hicho.
Imetolewa na Ofisi ya
Uhusiano
TANESCO Makao Makuu.
No comments:
Post a Comment