KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday, 12 May 2015

RAIS KIKWETE, AMTEUA MSUYA KUWA DCI


RAS Jakaya Kikwete, amemteua Kamishna wa Polisi (CP), Diwani Msuya, kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI).
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari, iliyosainiwa na Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi Ikulu, Premi Kibanga, kabla ya uteuzi huu CP Msuya, alikuwa Kaimu Kamishna wa kamisheni ya Intelijensia ya Jinai.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa Kamishna Msuya anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Robert  Manumba, ambaye amestaafu kwa mujibu wa Sheria.
Aidha, Rais Kikwete, pia amemteua Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), Valentino Mlowola kuongoza Idara ya Intelijensia ya Jinai, kujaza nafasi iliyoachwa na Kamishna Msuya.
Kabla ya uteuzi huu, DCP Mlowola alikuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza.
Uteuzi huu umeanza tarehe Mei 3 mwaka huu.





No comments:

Post a Comment