Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Fedha za Nje Bi. Doroth Mwanyika
akifugua Semina ya waandishi wa habari iliyoandaliwa na Mamlaka ya
Udhibiti na Ununuzi wa Umma PPRA katika kuelekea kuadhimisha miaka 10 ya
(PPRA) tangu kuanzaishwa kwake inayofanyika kwenye ukumbi wa Diamond
Jubilee jijini Dar es salaam, Semina hiyo inakutanishwa wawakilishi wa
Press Club za kutoka mikoa mbalimbali pamoja na waandishi wa habari
kutoka vyombo mbalimbali jijini Dar es salaam ikiwa ni pamoja na
mitandao ya kijamii, Maadhimisho yameanza leo mei 18/2015 na yataendelea
mpaka kilele chake Mei 20/2015.
Mwenyekiti
wa Bodi ya wakurugenzi ya PPRA Balozi Martin Lumbanga akizungumza
katika semina wakati akitoa salamu zake kwa wajumbe wa semina hiyo.
Baadhi
ya wakuu wa vitengo na maofisa wa PPRA wakiwa katika semina hiyo
inayofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.
Baadhi ya wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa PPRA wakiwa katika semina hiyo.
Wanahabari kutoka mikoa mbalimbali wakihudhuria semina hiyo.
NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dorothy Mwanyika, amesema sio kweli kama sheria ya manunuzi haifai kama baadhi ya watu wanavyojaribu kuuaminisha umma.
Dorothy, alitoa kauli hiyo,
wakati wa ufunguzi wa Warsha ya Elimu ya Manunuzi ya Umma kwa wadau wa habari
nchini, iliyoandaliwa na Mamlaka ya Manunuzi (PPRA), iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Alisema, kuwa wahusika
wakuu katika manunuzi wakizingatia sheria hiyo pamoja na kuweka uzalendo mbele,
anaamini hata utekelezaji wake utakuwa mwepesi ambao utalisaidia taifa katika
kudhibi matumizi yanayokwenda kinyume na sheria hiyo ya manunuzi.
Alisema, kuwamekuwa na
malalamiko mengi katika eneo hilo la usimamizi
wa manunuzi ya umma, chanzo cha malalamiko hayo yanatotokana uelewa mdogo juu
ya sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2011 na Kanuni zake za mwaka 2013,
ambazo ndizo hutumika kama mwongozo kwenye
manunuzi ya ummma.
“Baadhi ya watu wanadiriki
kusema kuwa sheria hii haifai kwa kuwa inachangia kuongeza gharama pamoja na
muda wa kufanya manunuzi serikalini,”alisema Dorothy.
Alisema, huo ni utetezi tu,
lakini ukweli ni kwamba Sheria hiyo na kanuni zake kiujumla zimeweza kiasi
fulani kuziba mianya ya ufujaji wa fedha iliyokuwa ikitumiwa hapo awali na
baadhi ya watu wasiokuwa waadilifu kwa Watanzania wenzao wakiwemo watumishi wa
umma na watu binafsi.
Dorothy, aliongeza kwa
kusema kuwa utekelezaji fasaha wa sheria hiyo unahitaji manunuzi kufanyika
katika mazingira ya uadilifu, uwazi, haki na ushindani mkubwa ili kuhakikisha
upatikanaji wa thamani bora ya fedha za umma zinavyotumika.
Akizungumzia wrsha hiyo ya
wanahabari, Dorothy, alisema kuwakutanisha wadau wote wabari nchini, anaamini
kuwa uamuzi huo umefanywa ili kutii Kaulimbiu ya maadhimisho hayo ya miaka kumi
ya PPRA, inayosema ‘Miaka kumi ya PPRA: Tumethubutu, Tumeweza, Tuendelee
kushirikiana kuboresha zaidi manunuzi ya umma.
Alisema lengo la kuandaa
warsha, hiyo ni kuwajengea uwezo zaidi wandishi na wadau wa habari juu ya
manunuzi ya umma pamoja na sheria na kanuni zinazoongoza sekta hiyo.
Dorothy, alisema kubwa
zaidi ni kukumbushana juu ya umuhimu wenu katika kutoa elimu sahihi ya masuala
ya manunuzi ya umma na hasa Sheria ya manunuzi ya Umma ya mwaka 2011 na Kanuni
zake za mwaka 2013.
No comments:
Post a Comment