KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday, 17 May 2015

ZUNGU: SINA MUDA WA KUPOTEZA KWA AJILI YA KUSHINDANA NA WASAKA TONGE KUPITIA JINA LANGU



MBUNGE wa Ilala, Mussa Azzan Zungu (CCM), amesema kuwa hana muda wa kulumbana na wanasiasa wanaosaka tonge kwa kutumia jina lake katika Wilaya ya Ilala.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Zungu alisema, baadhi ya watu wasiomtakia mema wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii hata kuchapisha vijarida vya magazeti  kwa lengo la kumchafua mbele ya wapigakura wake.
Zungu alisema kuwa hivi sasa amejikita katika kusimamia na kutekeleza ilani ya uchaguzi wa CCM na sio kulumbana na watu wanaotafuta ubunge kwa kutumia mitandao ya kijamii ikiwemo facebook.
“Unajua kuna mambo yanastaabisha sana kuna watu ambao ni wasakatonge wanahaha usiku na mchana eti wamchafue Zungu mara amekula fedha za Mfuko wa jimbo sh. milioni 400 tena hiki kijarida hicho kilika mwaka 2012 na sasa wamerudi tena,” alisema.
Alisema kuwa jimbo hilo haliwezi kupata kiasi hicho cha fedha kwa kuwa lina idadi ndogo ya watu huku kamati maalum inayoongozwa na mbunge ndiyo inahusika na fedha hiyo.
Zungu alisema wanasiasa wanaolitaka jimbo hilo hawapaswi kuwa na hofu kwa kuwa muda ukifika wanatakiwa kujitokeza ili wakutane uwanjani kwa kuwa waamuzi ni wapigakura

No comments:

Post a Comment