KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Monday, 1 June 2015

MAKONDA: TANZANIA HAKUNA TATIZO LA AJIRA

MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda, amesema Tanzania haina tatizo la ajira ila kuna tatizo la fikra.
Kauli hiyo inakuja baada ya baadhi ya watia nia wanaomba ridhaa ya kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika kugombea nafasi ya uraisi kwenye uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, kueleeleza kuwa tatizo la ajira kwa vijana ni sawa na bomu linalosubiri kulipuka.
Makonda alitoa kauli hiyo, mwishoni mwa wiki wakati wa uzinduzi wa maonyesho ya tano ya Tanzania Homes Expo yaliyoandaliwa na Kampuni za  EAGgroup jijini Dar es Salaam.
Alisema Tanzania ina rasilimali nyingi lakini vijana wamekuwa hawazioni fursa ambazo zingeweza kuwapatia ajira  na kuondokana na kuilaumu Serikali.
“Tanzania ina rasilimali nyingi ambazo kama vijana  wangezitumia  zingeweza  kuwapatia ajira na  kuondokana  kukimbilia nchi jirani kujihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya na kuishia kutofikia malengo yao.”alisema Makonda.
Alisema fursa hizo zimekuwa zikichangamkiwa na wageni ambao wanatengeneza malighafi kwa kutumia rasilimali za hapa nchini.
“Vijana wengi wanakimbilia nje ya nchi wanaziacha fursa  na kushindwa kukuza uchumi wa nchi” alisema Makonda.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Kampuni za EAGgroup, Imani Kajula, alisema maonyesho ya Tanzania Homes Expo lengo lake ni kutoa elimu kwa jamii ili  ielewe usuluhisho mbalimbali wa makazi yao.
Kajura aliongeza kuwa lengo kubwa la Tanzania Homes Expo ni kuweka jukwaa moja la mtu anayetafuta usuluhisho wa nyumba  kuanzia Ulinzi  na kudai kuwa Watanzania wengi hawajui njia za kuweka maeneo yao ya makazi yakawa katika hali ya usalama
“Jinsi Nchi yetu inavyozidi kukua, kunahitajika watoa huduma mbalimbali kwa sababu kumekuwa na ongezeko la watu wanaohitaji huduma  mbalimbali za makazi yao.
makazi tukaona ni muhimu kuwa na sehemu  ambayo watoa huduma na wahitaji huduma wanakutana kwa pamoja.
Maonyesho haya yanashirikisha washauri wa masuala ya ujenzi, wajenzi wa majengo na nyumba za kuuza, kampuni za bima, wanaoendeleza viwanja, Kampuni za fedha pia suala la Afya lipo.”alisema  


No comments:

Post a Comment