KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday, 17 July 2015

PAMBA AKABILIWA NA UPINZANI MKALI JIMBONI KWAKE



MBUNGE wa Pangani Tanga, Salehe Pamba,  anakabiliwa na upinzani mkali katika kutetea jimbo hilo kutokana na kujitokeza wanachama wenzake nane wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwani kuteuliwa na chama hicho ili kupeperusha bendera ya chama hicho katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Wakati wakichukua fomu, wanachama hao kila mmoja alisema kuwa amesukumwa na nia ya kutaka kupigania matatizo ya wananchi.
Akizungumza kwa njia simu kutokea Pangani jana,  John Semkhande, ambaye ni diwani anayemaliza muda wake katika kata moja wilayani humo, alisema msimu huu CCM inategemea kupata wagombea wengi zaidi ya hao.
Aliwataja wanachama hao waliojitokeza kuwa ni Salehe Pamba ambaye ndiye mbunge wa sasa, Rosemery Alfred, Juma Aweso, Ayoub Mswahili na Halima Kimbau.
Wwngine ni Rished Mohamed ambaye aliwahi kuwa mbunge kwa kipindi cha miaka 15, Abrahaman Magati, Omary Chanbega na Elzabeth Alatanga.
Akizungumzia kujitokeza kwa wanachama wengi kinyume na miaka awali, Senkhande, alisema hiyo ni kuonesha ni jinsi gani wanachama hao walivyoshikwa na hamu ya kuwasogezea maendeleo wananchi.
“Unajua mimi kwa taaluma ni mwandishi wa habari na mwanachama wa CCM, lakini kujitokeza kwa wanachama hao katika kuwania nafasi hiyo, huenda kuna mambo wameona hayakwenda sawa au ni utaratibu tu, kwami uongozi ni sawa na mbio za kijiti na inafikia wakati lazima alyoko madarakani  amkabidhikijiti kwa mwingine,”alisema Semkhande.

No comments:

Post a Comment