Mkurugenzi Takwimu za Jamii na Sensa ya
Watu na makazi, Ephraim Kwesigabo amesema mfumuko wa bei wa mwezi julai
umeongezeka kwa asilimia 0.4 kutoka asilimia 0.2 ya mwezi juni mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, ongezeko hilo limetokana na kuongezeka kwa bei za baadhi ya bidhaa za
vyakula na zisizo za vyakula .
Alizitaja baadhi ya bidhaa hizo za
vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko wa bei pamoja na asilimia zake
ndani ya mabano, kuwa ni unga wa mahindi (2.5), ulezi (2.5), samaki (4.8),
viazi vitamu (2.6) na ndizi za kupika (3.4).
Kwesigabo alisema kwa upande wa bidhaa
zisizo za vyakula ni gesi ya kupikia (3.7), dizeli (5.9) na petroli (4.9).
Aidha, mfumuko wa bei kwa nchi jirani
umeongezeka kutoka asilimia 4.9 hadi 5.4, kwa Uganda ambapo nchini Kenya
umepungua kutoka asilimia 7.03 hadi 6.62.
Hata hivyo, Kwesigabo alisema thamani
ya shilingi ya Tanzania imefikia shilingi 62.na senti 98 julai mwaka huu
ikilinganishwa na septemba 2010.
No comments:
Post a Comment