Wakazi hao, waliyasema hayo wakati walipozungumza na
mwandishi wa SAUTI PEVU jijini jana, kwamba hivi sasa wanaishi kwa
wasiwasi kila linapoingia giza.
Walisema eneo hilo la Kibamba hivi sasa limekumbwa na
vitendo vya uhalifu kutokana na vijana wengi waliyokimbilia huko kujificha
baada ya kufanya uhalifu katika maeneo mengine jijini.
“Hawa vijana wanaotusumbua wengi wao ni wale waliyofanya
uhalifu katika maeneo mengine ambako wanatafutwa ili wafikishwe kwenye vyombo
vya sheria lakini cha kushangaza baadala watulie lakini ndiyo kwanza
wanaendelea na uhalifu wao tunawajua mmoja mmoja,”alisema mmoja wa wakazi hao
huku akiungwa mkono na wenzake.
Walisema, baadhi ya vijana hao wapo wanatoka manzese,
wakiiungana na wengine kutokea Maili Moja mkoani Pwani.
Pia walisema vibaka hao wamekuwa wakijeruhi wakazi wa
maeneo hayo wakati wanapovamia nyumba, kwa lengo kupatiwa kile wanachohitaji.

No comments:
Post a Comment