SERIKALI imetakiwa kuchunguza mkataba wa muwekezaji katika
Hotel ya Embasy ili kubaini kama ameshindwa kuiendeleza basi irudishwe
serikalini kwa ajili ya masilahi ya Taifa.
Wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka jana, Rais John
Magufuli, aliahidi kurudisha viwanda ma maeneo mengine ambayo wawekezaji wake
wameshindwa kuyaendeleza huku wemgine wakigeuza kazi za mikataba
waliyokubaliana na serikali.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kivukoni wilayani Ilala
jijini Dar es Salaam, Gesper Makame aliyasema hayo jana, wakati alipokuwa
akizungumzia taarifa za kuwa muwekezaji katika hotel hiyo, ameanzisha gereji
bubu ambayo inadaiwa kuwa kero kwa baadhi ya ofisi za jirani.
Alisema hayo baada ya wakazi wengi wa mtaa huo kuhoji kuwa
inakuwaje mradi wa kuendeleza hoteli hiyo unaendeshwa kwa kusuasua na umechukua
muda mrefu, huku wakidai kuwa eneo hilo hivi sasa limegeuzwa kuwa gereji bubu
kinyume cha sheria.
Hata hivyo, Makame, alisema hatua hiyo ya kuiresha
serikalini itafuatia baada ya serikali kuchunguza na kujiridhisha kama muwekezaji
huyo ameshindwa kutekeleza vigezo vya mkataba
aliyoingia ns serikali.
“Nikweli nilipokea malalamiko hayo kuwa pale kumeanzishwa
gereji bubu hali iliyonifanya niende na kukutana nawasimamizi wa hoteli hii
ambao tulikubaliana kuwa wasingeendelea na utaratibu huo, nikweli kuna gari
nimeiona ambayo bodi yake ilikuwa ikitengezwa.
“Kwanza ni kinyume cha sheria isitoshe jirani zao
wanalalamika kuwa wanawasumbua kwa kelekele wakau wamatengenezo hayo ya magari
hivyo kuwafanya wakose utulivu wa kutekeleza majukumu yao,”alisema Makame.
Alisema kutokana na mazungumzo hayo, aliamini kuwa
hawangeendelea tena, sasa kama wanaendelea kama inavyodaiwa na majirani zao
basi atayafanyia kazi madai hayo.
Naye Ofisa Utawala wa Kampuni ya Wellworth Group, ambao ndiyo wamiliki wa Hoteli hiyo, Simon Nguka, alisema madai hayo hayana ukweli
wowote, kwamba madai hayo yanalengo la kutaka kuupotosha umma kuhusu mradi
mkubwa ambao utakuwa chanzo kizuri cha mapato kwa taifa.
“Magari yaliyoko pale ni ya kampuni kwa hiyo siyo kweli
kama kuna gereji bubu, hizi taarifa hazina ukweli waowote na waliyozitoa
hawajui chochote kuhusu kinachoendelea pale,”alisema Nguka.
Pia, alipinga na kuwashangaa wanaodai kuwa huenda kuchelewa
kukamilika kazi ya ujenzi huo kumetokana na wamiliki wake kuzitumia hati za
umiliki wa jengo hilo kwenda kukopa fedha kisha kuzitumia katika miradi yao
mingine, na kuwataka wenye ushahidi wa hilo waupeleke serikalini.
Alisema hakuna kitu kama hicho kinachoendelea ni majungu
kutoka kwa watu ambao hawana ufahamu na
uwekezaji huo, ambapo naamini serikali ndiyo inajua ukweli wa uwekezaji huo.
MWISHO
No comments:
Post a Comment