WAZIRI Mkuu Kasim Majaliwa ameitaka Bohari ya Dawa nchini
(MSD), kuwa inahakikisha inavifikisha salama msaada vifaatibaa vyenye thamani
ya zaidi ya Sh. Bilioni 10, ambavyo vimetolewa na Kampuni zinazozalisha
vinywaji baridi kwa ajili ya hospitali za mikoa 14.
Hata hivyo hafla hiyo iliingia dosari baada waziri mkuu kuzuiliwa
na wafanyakazi wa PSI asiondoke hadi asikilize kilio chao cha manyanyaso
wanayofanyiwa na uongozi wao.
Majaliwa aliyasema hayo wakati wa hafla fupi ya makabidhiano
ya vifaatiba hivyo, kwamba vimekuja katika wakati muafaka kwani msaada huo
utasaidia katika kukabiliana na upungufu wa vifaa na vifaatiba vya kutolea
huduma za afaya.
Msaada huo umetolewa na Kampuni zinazotengeneza vinywaji
baridi ambazo ni Coca Cola Kwaza (T), Nyanza Bottlers; Bonite; Kampuni ya
SBC-Pepsi (T); Kampuni ya SSB (Azam) na nyingine.
Alisema lengo la msaada huo ni kwenda kwenye vituo
vilivyokusudiwa kwa hiyo serikali haitakubali kuona baadhi ya watu wasiyokuwa
waaminifu wanavuruga mpango uo kwa kuviharibu au kuiviiba kwa masilahi binafsi
“Niambiwa vifaa na vifaatiba vitakavyokabidhiwa vina thamani
ya shilingi bilioni 10 za kitanzania ambayo ni makontena 20 yenye refu wa futi 40
kila moja ambayo ndani yake kuna makasha zaidi ya 1,500 ya vifaa vipya kabisa
na vingine zaidi ya 300 vikiwemo vitanda 80 na magodoro yake.
“Msaada huu ni mkubwa ambao haujawahi kutokea katika sekta
ya Afya, napenda kutumia fursa hii kusistiza kwamba serikali kupitia MSD,
itahakikisha vifaa hivi vinasambazwa kwenda kwenye vituo husika kwa umakini
mkubwa ili viweze kutumika kama ilivyokusudiwa”alisema Majaliwa.
Aliyataja orodha ya maeneo ambayo yana upungufu wa vifaa na
vifaatiba, ambako wanatarajia kuvipeleka kuwa ni Mikoa ya Dodoma, Geita,
Katavi, Kilimanjaro, Kigomana naLindi.
Mingine ni Mara, Mbeya, Mtwara, Shinyanga, Tanga, Tabora na
Rukwa huku akibainisha kuwa kutokana na mzigo huo kuwa mkubwa anaamini kuwa
mikoa yete iliyobaki ya Pwani, Singida, Iringa yote inaweza kupata.
Aidha, Majaliwa alisema kindo hicho ni ishara kuwa
mabadiliko nmakubwa yanaweza kutokea nchini, ikiwa serikali na sekta binafsi
watafanya kazi pamoja kam ilivyojitokeza.
Majaliwa, aliongeza kwa kusema kuwa serikali itaendelea
kuboresha uhusiano na ushirikiano na sekta binafsi katika kuwaletea maendeleo
wananchi.
Wafanyakazi
wampokea kwa mabango
Wakati akiwa anaondoka kundi kubwa la wafanyakazi
wakiongozwa na mtu mwenye ulemavu, walifunga barabara kuzui waziri ili aseme
chochote kuhusu haki zao ambazo zinafinyangwa.
Waziri Mkuu baada ya kuzuiwa ilibidi shuke kwenye gari ili
kuwasikiliza, ndipo kiongozi wa wafanyakazi hao, Amin Athuman alipoanza kueleza
uneovu wanaofanyiwa.
Alisema kuwa wamekuwa wakifanya kazi kwa muda mrefu bila ya
kupewa mikataba huku wanacholipwa hakiendani na kazi wanazofanya.
“Hapa sisi kila tunapodai haki zetu tunatishiwa kufukuzwa
kazi, hatuna PPF kwa Ujumla uongozi ni mbovu kwani hata usalama wetu kaazini
uko mashakani tuna kuomba utusaidie kwa vile serikali yako imeonesha kusaidia
wanyinge na tuna imani nayo,”alisema Athuman.
Baada ya kumaliza kuelezea kero zao, Majaliwa, aliwataka
wafanyakazi hao wafifike kazini leo ya kukosa kwani atamwaaiza waziri mwenye
dhamana Jenista Mhagama afike ofisini hapo kwa ajili ya kuwasikiliza.
“Mmsema hamna makato ya PPF, niwaahidi hidi kuwa kesho
(leo), atakuja kulishughulikia tatizo lenu na kwa kawaida hatucheleweshi
kumaliza matatizo, kwamba matatizo yenu
yote yatapatiwa ufumbuzi hapo hapo,”alisema Majaliwa.
Alipomaliza kusema hayo aliwaomba wampishe ili apate
kuondoka, bila kipingamizi alipishwa na kuendelea na safari.
Awali, Mkurugenzi wa MSD, Laurean Bwanakunu, alisema
anazishukuru kampuni hizo kwani zimekuwa mfano wa kuigwa huku akibainisha kuwa
MSD imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na kampuni ya Coca Cola kwa muda mrefu
sasa.
Alisema licha ya kampuni hizo kutoa msaada huo bado pia
zimeahidi kutoa msaada wa mafunzo kwa watanzania watakaosimamia vifaa hivyo kwa
gharama zao.
Pia, aliiomba serikali kiongezea bajeti ili iweze kusimamia
mipango yake ya kuboresha huduma za afya nchini.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Coca Cola Kwanza, Basil
Gadizios, aliipongeza serikali katika hatua zake za kupambana na vitendo vya
rushwa nchini.
Alisema hali hiyo itaweza kuifanya Tanzania ifanikiwe
katika kuwaletea wananchi wake maendeleo.
MWISHO
No comments:
Post a Comment