KAMATI ya Bunge ya Ukimwi imeibu
madudu katika Hospitali ya Mwananyamala baada ya kubaini kitanda kimoja
hutumika kulaza watoto 15 kwa wakati mmoja.
Kaimu Mganga Mkuu Delila
Mushi alieza hayo mbele ya Kamati hiyo wakati ilipofanya ziara ya kushtukiza
kataika Hospitali hiyo jijini Dar es Salaam jana.
Akizungumza kwa hisia mbele
ya Kamati hiyo Dk Delila alisema katika wodi ya watoto kuna vitanda 18 ambapo watoto wachanga 150 hulazwa katika vitanda
10 sawa na watoto 15 kitika kila kitanda kimoja.
“Wakati watoto hao wakilala
kitandani wazazi wao wanalala chini jambo ambalo linatusikitisha,”alisema
Delila.
Alisema hali hiyo
imechangiwa wodi ya watoto kukosa nafasi ya kuongeza vitanda kwa vile hakuna
nafasi kwa muda mrefu sasa.
DK. alisema katika vitanda
hivyo 18, kuna vitanda nane vimetengwa kwa ajili ya watoto njiti.
“Hili suala tayari
tumekwisha liandikia barua kwa muda mrefu lakini hadi sasa bado tunasubiri
utekelezaji kutoka serikalini,”alisema Dk. Delila.
Dk. Delila, alisema nafasi
ya kujenga jengo jipya ipo na baadala yake imekuwa ikitumia majengo ya zamani
ambayo hayo hayaendani na ongezeko la wakazi.
“Hivi sasa hospitali hii
inakabiliwa na uchakavu wa miundombinu ya majitaka hali inayosabisha kufurika
na kusambaa harufu katika hospitali hiyo,”alisema Dk. Delila.
Aidha, Dk. Delila, alisema pia
wanakabiliwa na tatizo la mashine ya kuchakata takataka kwani iliyopo uwezo
wake ni wa kuchakata kilo 120 huku hospitali hiyo ikizalisha kilo 200 kwa siku.
Alisema gharama ya kununua
mashine hiyo ni sh. milioni 100.
Alitaja changamoto nyingine
kuwa ni uhaba wa wafanyakazi ambao ni tatizo kubwa linalo ikabili hospitali
hiyo kwa muda mrefu sasa.
Akizungumzia Changamoto
hizo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Husna Mwilima, alisema ingawa ziara yao
ilikuwa ikilenga zaidi kutembelea kitengo cha dawa za kulevya, hata hivyo suala
la afya ni la kila mdau kwa hiyo wanamuahidi kuwa watalifuatilia suala hilo.
“Kwa kweli jambo hili
limetusikitisha, kwa ulivyolizungumzia inaonesha ni jinsi gani unavyoumia na
kutufanya hata sisi tujisikie huzuni kwa hiyo Kamati yetu itahakikisha ufumbuzi
wa matatizo yote hayo yanapatiwa ufumbuzi wa haraka,”alisema Husna.
Kwa upande wake Dk. Hassan
Nyandindi, alisema tangu kuanzishwa kitengo cha Methadine mwaka 2012, hivi
sasakitengo hicho kinahudumia waathirika 1110 kati ya hao wanawake ni 179.
Kwaa upande wa hospitali ya
Taifa ya Muhimbili katika Kitengo cha Mihadarati, Dk. Jessie Mbwambo, alisema
wasichana wako wanaotumia mihadarati wako hatarini kuambukizwa na kuambukiza
ugojwa wa ukimwi kwa vile wamekuwa wakifanya mapenzi na wanaume 60 kwa mwezi.
Alisema kutokana na matumizi
hayo ya dawa za kulevya wanawake hao wamejikuta wakiingia katika vitendo hivyo
bila ridhaa yao.
Alisema kutokana na
mazingira hayo, inafanya wasichana hao kuwa chanzo cha maambukizi mapya ya Ukimwi.
Naye Naibu Waziri Ofisi ya
Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Dk. Abdallah Possi,
alisema ili kupambana na matumizi ya mihadarati kuna haja ya Wabunge kuisaidia
serikali kuwafichuwa vigogo wanaohusika na biashara hiyo.
"Ni waombe bajeti ya wizara yetu itakapowasilishwa bungeni muingune mkono ili kuondoa matatizo katika sekta ya afya,"akisema Dk.Possy.
Vilevile aliwatahadhalisha wabunge kuwa wanaweza kujikuta wanashindwa kuwataja baadhi ya wafanyabiashara wanaowasaidia labda nyakati za kampeni hivyo kujikuta wakipatwa na kigugumizi cha kuwataja kwani baadhi yao ndiyo hao hao wanaojihusisha na biashara hiyo haramu.
Pia alisema matatizo yote
yaliyoainishwa na Vitengo hivyo vya dawa za kulevya yani kile cha Muhimbili na
Mwananyamala, ameyachukua na kwenda kuyafanyia kazi kwa kushirikiana Wizara ya
Afya.
Pia aliwakumbusha wabunge hao kuwa mipango ya serikali ya awamu ya tano ni kuondokana na bajeti tegemezi.
MWISHO
No comments:
Post a Comment