KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Saturday, 26 March 2016

KIVUKONI WALALAMIKA KUKOSEKANA 'DUSTIBIN' ZA KUHIFADHIA TAKATAKA

UKOSEFU wa ‘dustibin’ za kuhifadhi takataka katika mitaa mbalimbali ikiwemo Kivukoni jijini Dar es Salaam, kumekuwa chanzo cha mlundikano wa takataka kwenye mitaa hiyo.
Mwenyekiti wa Serikali yaMtaa wa Kivukoni, Gasper Makame, aliyasema hayo wakati aliposimamia kazi ya usafi katika mtaa huo, inayofanyika kila wiki ya mwisho ya kila mwezi.
Utaratibu huo ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli, la kubalisha  Siku ya Desemba 9 kuwa ya Usafi baadala ya kuwa Siku ya maadhimisho ya Uhuru.
Makame, alifikia hatua hiyo baada ya wakazi wa mtaa huo waliyokusanyika kwa ajili ya kufanya usafi kulalamika kuwa wanakabiliwa na tatizo la dustibin za kuhifadhia takataka zinazozalishwa kila siku.
“Hicho wanachosema wananchi ni sahihi kinachotakiwa hapa, tuhamasishe wale wenye uwezo na wale ambao hawana uwezo na tusaidiane  angalau tuweke sh 200 kwa kila mmoja wetu ili tupate dustibin, dustibin ni shida na tatizo kweli,”alisema Makaeme.
Hata hivyo, Makame alisema pamoja nakazi hiyo ya usafi kwenda vizuri lakini bado wanakabiliwa na tatizo la kufanyia usafi katika kipande cha mita 60 ambacho kiko chini ya Bandari kwa vilekiko ndani ya uzio wao.
Alisema kipande hicho kiko ufukweni mwa bahari ambapo kimezunguushiwa uzio ambao unawafanya washindwe kuingia bila ya idhini ya uongozi huo wa Bandari.
“Tulifika pale tukashindwa kuingia lakini kwa vile kile kipande ni chao basi ni vema wakaonesha mfano kwa kukiweka katika hali ya usafi, lakini kuna baadhi ya vijana wanaokaa pale (Mateja), wenyewe wanaiomba bandari iwaletee vifaa wapkifanyie usafi,”alisema Makame.
Aidha, alisema wauza matunda kwa mikokoteni wamekuwa kero kubwa katika mtaa huo, kwani wamekuwa chanzo cha uzalishaji wa takataka ambazo baada ya shughuli zao huzitekelekeza na kuzifanya zinaoza na kusabisha harufu mbaya katika maeneo husika.
Makame, alisema katika kukabiliana na tatizo hilo, hadi sasa wamefanikiwa kukamata baadhi ya wafanyabiashara katika eneo la Motel Agip na kuzuia mikokoteni yao katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa kwa ajili ya kuwachukulia hatua za kisheria.
Kuhusu kupigwa marufuku matumizi ya pombe inayojulikana kwa jina la Viroba, kutokana na vipakti vyake kuzalisha uchafu, Makame alisema inategeme kauli ya uongozi wa juu kwa vile watakaposema wao serikali ya mtaa kwa kushirikiana na wananchi hilo litafanikiwa     
Awali wakazi wa mtaa huo waliomba serikali isambaze dusbin nyingi katika mitaa ambazo zitawafanya wananchi kutupa takataka zao humo huku piawakiomba kupigwa marufuku pombe ya kiroba ambayowamedai vifungashio vyake vimekuwa vikichafua mazingira kwa kiasi kikubwa.

No comments:

Post a Comment