KATIBU Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa, amesema Tanzania inayo nafasi kubwa
ya kupata mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka nchini Uganda hadi katika
bandari ya Tanga ukilinganisha na nchi nyingine zilizoko katika Jumuiya ya
Afrika Mashariki.
Profesa Ntalikwa, alisema
hayo, baada ya makubaliano kati ya Tanzania na Uganda, ya kujenga bomba hilo
lenye urefu wa kilomita 1,410; Kenya ikaibuka na kuanza kufanya mikakati kwa
kasi ya ajabu wakitaka mradi huo upitie bandari ya Lamu.
Kama hiyo haitoshi, Katibu
Mkuu wa wa Nishati wa Kenya alikamatwa na maofisa Uhamiaji mkoani Tanga baada
ya kujaribu kujipenyeza kwenye ujumbe wa Waziri wa Nishati wa Uganda, uliyokuja
nchini kuangalia mazingira ya utekelezaji mradi huo bandani Tanga.
Akizungumza na wandishi wa
habari nje ya mkutano kati ya Wizara hiyo na wafanya biashara wa Sekta ya mafuta
nchini, ambao ulifanyika jijini Dar es Salaam jana, Profesa Ntalikwa, alisema lengo
la kukutana na wafanyabiashara hao ni kuwatangazia fursa zinazoweza kupatikana
katika mradi huo mkubwa.
Alisema kujengwa mradi huo, kunatokana
na mazingira ya Tanzania ikiwemo usalama katika ardhi yake, yanatoa fursa kubwa
kufanikisha mradi huo ukilinganisha na nchi nyingine.
“Tanzania ina uzoefu wa
kuendesha miradi mikubwa kama hiyo, mfano ni miradi ya mabomba manne gesi ambayo
tunayo kwa sasa,”alisema Profesa Ntalikwa.
Pia Profesa Ntalikwa,
alisema vigezo vyote vinavyohitajika katika ujenzi huo ikiwemo bandari yenye
kina kirefu ipo katika mkoa huowa Tanga linako tarajiwa kujengwa.
“Ujenzi wa mradi huu
utagharimu sh. Bilioni nne hadi kukamilikakwake kwani unatarajiwa kuanza mwaka
ujao kisha kukamilika ndani ya miezi 36,”alisema Profes Ntalikwa.
Akizungumzia kushirikishwa
wafanyabiashara hao Profesa Ntalikwa, alisema lengo la kukutana nao ni
kuwatambulisha fursa nyingi za kibiashara, ambazo zitapatikana katika mradi
huo.
“Mradi huu ni mkubwa na una
manufaa makubwa kiuchumi kwa taifa hivyo, ni lazima kila mfanyabiashara na raia
kwenye nafasi yake ungane na serikali kuhakikisha hautoki mikononi mwetu kwani
tayari mkuu wan chi ameonesha dhamira ya dhati kuhakikisha Tanzania inasonga
mbele,”alisema Profesa Ntalikwa.
Alitaja faida hizo za
kiuchumi kuwa ni upatikanaji wa zabuni kubwa, utazalisha ajira, kodi mbalimbali
ambazo zinaweza kupatikana lakini bomba hilo litakuwa na faida na faida
kuchechemua pato la nchi.
Mwenyekiti wa
Wafanyabiashara hao, Gideon Kaunda, alisema baada ya mkutano huo watasafiri
kwenda nchini Uganda kukutana na Rais Yoweli Museven kumuelezea kuwa Tanzania
ndiko sehemu ambayo inaweza kujengwa bomba hilo.
Alisema kuwa wafanyabiashara
wote wa sekta ya mafuta nchini
wamejidhatiti kwa ajili ya kupokea mradi huo na hawako tayari kuponyokwa,
kikubwa wanaomba ushirkiano kati yao na serikali ili kukamilisha adhima ya
mradi huo.
No comments:
Post a Comment