KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday 12 July 2015

VIJANA WAMSHAURI JANUARI MAKAMBA ASIKATE TAMAA

Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akiwa na aliyekuwa mgombea wa nafasi ya urais, January Makamba, ambaye alifanikiwa kuingia kwenye wagombea watano kati ya 38 waliyojitokeza kuwania nafasi hiyo.
BAADHI ya vijana mkoani Dar es Salaam, wamemtaka Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia, January Makamba kutokata tamaa baada ya kukosa nafasi ya kuteuliwa kuwa mgombea wa nafasi ya urais ndani ya Chama Chama Mapinduzi (CCM).
Vijana hao walisema hivyo, baada ya kukamilia mkutano wa kumpata mgombe wa nafasi hiyo ndani ya chama hicho,  mjini Dododoma jana, ambapo Dk. John Magufuli ameteuliwa kupeperusha bendera ya CCM itakapopambana na wapinzani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Wakizungumza na Tanzania Daima jijini, kwa nyakati tofauti jana, vijana hao, walisema kwa hatua aliyofika ya wagombea watatano kati ya 38, katika uteuzi huo inaonesha dhahiri kuwa Watanzania wanahitaji uongozi wa kizazi kipya.
Walisema, hivyo kwa vile wanaamini kuwa uwezo wa kuongoza nchi hii anao, kilichochangia akose nafasi hiyo ni kutokana na umri wake mdogo, ambao baadhi ya wajumbe waliopewa dhamana ya kuteua kuangalia zaidi umri wa mgombea, akibainisha mwenye umri mkubwa huwa ndio wananmpa nafasi zaidi.
Stephen James mkazi wa Gongolamboto, alisema kuwa Makamba, hana haja ya kusikitika na kukata tamaa kwa vile umri wake bado unaruhusu kugombea nafasi hiyo panapo maajiliwa ifikapo mwaka 2025 kwani atakuwa na miaka 51, cha msingi ajipange kuanzia sasa.
“Nafarijika kumuona Makamba akiwa hazina kubwa ndani ya CCM hivyo umefika wakati kwa wakongwe wa chama hicho kuwaamini vijana kwa vile wakiaminiwa na kuthaminiwa uwezo wao, kutoka ngazi ya chini hadi taifa wanaweza kufanya mambo makubwa nchini,”alisema James.
Halima, Kisambu, alisema lazima wazee wa chama hicho wabadili msimamo katika kuachia nafasi za uongozi kwa kizazi kipya bila ya mizengwe hali itakayowafanya vijana wote wa CCM na wengine kuamini kuwa chama hicho ni chao wote.
Hivi karibuni Naibu Waziri huyo, alikaririwa navyombo vya habari, akisema hana kinyongo na anawaheshimu  baadhi ya wagombea na yuko tayari kufanyakazi na mgombea yeyote kwa ajili ya kuendelea kukijenga na kukiimarisha Chama chao na kutatua changamoto za Watanzania.


No comments:

Post a Comment