KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday 23 August 2015

UHAKIKI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA JIJINI DAR LAOTA MBAWA

Mgombea ubunge Jimbo la Kawe, Mdee

Mgombea wa ubunge Jimbo la Ubungo, Kubenea
WAGOMBEA ubunge kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Halima Mdee (Kawe), Saed Kubenea (Ubungo), wameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), itangaze kuwa ni lini zozi rasmi la uhakiki wa Daftari la Wapiga kura linaanza jijini Dar es Salam.
Halikadhalika wameitaka kumaliza kasoro mbalimbali zilizojitokeza katika maeneo mengine nchini.
Wakazi jijini walijiandikisha katika Daftari la Wapiga Kura kwa kutumia mfumo wa kieletroniki Biometric Voters Registration (BVR), kuanzia Julay 22 hadi Ogasti 4 mwaka huu.
Wakizungumza na waandishi wa habari jijini jana, wagombea hao walisema kuwa baada ya kujiandikisha, zoezi hilo la uhakiki, lilitakiwa kuanza Ogasti 18 mwaka huu lakini hadi sasa halijaanza na hawajui kinachoendelea.
Mdee, alisema wakiwa wadau wauchaguzi wamebaini kuwa hadi sasa wapiga kura wao hawajahakikiwa katika maeneo, hali inayowatia shaka,  kwa vile hata madaftaari yenyewe hayajafika katika Halmashauri na Kata kwa ajili ya ukaguzi.
“Sasa tunaitaka NEC ieleze kwa kina na kidagaubaga kuwa ni lini haswa zoezi la uhakiki wa daftari hilo utaanza,”alisema Mdee.
Mdee, pia aliitaka NEC kutoa maelekezo kwa wasimamizi wa uchaguzi kuwa madaftari ya majina yote ya wapiga kura ya pelekwe kwenye vituo waliko jiandikisha baadala ya kuwataka waende katika ofisi ya Kata.
“Itakuwa ni vigumu kwa wananchi wa vituo vyote katika Kata husika kwenda kukagua majina yao kwenye ofisi za kata, jambo ambalo halitawezekana kwa vile siku zenyewe zilizopangwa ni chache, kutakuwa na mkusanyiko mkubwa, hivyo ni vyema majina hayo yakapelekwa na kubadikwa kwenye vituo vyao.
“Ni rai yetu mashine za BVR zikawekwa karibu na mitaa kwamba endapo kutabainika kasoro katika vituo husika basi ziweze kushuhulikiwa haraka ,”alisema Mdee.
Aliongeza, kwa kuiambia NEC kuwa wao wakiwa wagombea wa mkoa huo hawatakubali kuona wapiga kura wao wanakukosa haki yao ya kupiga kura kutokana na uzembe wa tume.
Akizungumzia kasoro zilizojitokeza katika maeneo mengine nchini ambako tume imekwisha hakiki majina nchini Mdee, alisema kuwa kuna baadhi ya wapiga kura majina yao hayakuonekana.
Alisema kuna maeneo ambako watu wamejiandikisha zaidi ya 3000 lakini cha kushangaza baadhi ya majina hayako katika daftari lakini wananchi hao wanavyo vitambulisho (vichinjio), vyao.
“Unajua uchaguzi wa safari hii unaupinzani mkali sasa kukosekana kwa wapiga kura kiasi chochote ni jambo la hatari sana,”alisema Mdee.
Alisema, kuna mchezo mchafu unaofanywa na wakurugenzi hivyo wanaitaka tume hiyo kuhakikisha kuwa inamaliza kasoro hizo haraka, ambazo zinaweza kuja kuwanyima haki ya kupiga kura wananchi nakuzua vurugu.
 

Naye Kubenea, alisema kuwa ziko taarifa zinazodai kuwa kuna mpango wa wizi wa kura kwa kuongeza idadi ya kura za urais na udiwani, ambapo mpango huo unaratibiwa na baadhi ya watendaji wa NEC, ambao siyo waadilifu.
“Tunashangaa kuwa hadi sasa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum kuwa hadi sasa hawajamsikia akitoa kalipio kali kuhusu shahada hizo kali kwa kutumia itelejensia kwa watu hao wa CCM wanaodaiwa kuwa na shahada hizo,”alisema Kubenea.
Alisema kuwa hadi wakati huu wakielekea katika uchaguzi huo wana mashaka na tume kwasababu baadhi ya viongozi wa tume hiyo uwadilifu wao unatiliwa shaka katika kusimamia kazi hiyo.
Kubenea, alisema kutokana na wasiwasi huo wanamtaka Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damiani Lubuva, ili aondoke vizuri katika ofisi hiyo ni lazima asimamie sheria na ahakikishe kuwa uchaguzi huo unakuwa huru na haki.
“Kama alivyosema mwenzangu hawatakubali kwa wapiga kura wao waliokesha, na miswaki, ndoo za maji, vyungu, pawa, nyungo ili kusubiri kujiandikisha leo wasipige kura huku wakiwa wamejiandikisha,”alisema Kubenea.
Alisema vinginevyo mafuriko au maporomoko ya wananchi waliyokuikataa CCM kama watanyimwa haki yakupiga kura na NEC basi itambue kuwa itaingiza nchi katika machafuko.

MWISHO


No comments:

Post a Comment