KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday 27 February 2015

NDEGEVITA YA JWTZ YAANGUKA



JESHI la Wananchi wa Tanzania  (JWTZ), limesema ndegevita moja imeanguka katika uwanja wa ndege wa kijeshi uliyoko Mwanza wakati zikifanya mazoezi ya kivita.

Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es salaam leo, Meja wa Jeshi hilo, Joseph Masanja, alisema ndegevita hizo zilikuwa katika mazoezi ya kwaida ya kivita.

Alisema ajali hiyo ilitokea wakati rubani wa ndege hiyo Meja Piter Lyamungu alipokuwa akijiandaa kuruka, ilitokea ndege nyingine (ndegemnyama), ikaingia katika  moja ya injini zake na kusababisha ndegevita kuwaka moto.
Meja Masanja, alisema hata hivyo rubani wa ndegenita hiyo alipoona ndege yake inawaka moto alifanikiwa kujirusha nje ya ndege hiyo kwa kutumia vifaa maalumu.

Alisema baada ya kutumia vifaa hivyo alifanikiwa kuokoa maisha yake ingawa amepata majeraha katika mguu wake wakati kujiokoa.
Meja Masanja, alisema hali ya rubani huyo inaendelea vizuri na anaendelea na matibabu ya kawaida.

Alitoa rai kwa wananchi kuwa wasiwe na hofu kwani ajali iliyotokea ilikuwa ni ajali ya kawaida na kwamba waendelee na shughuli za kama kawaida.

Meja Masanja aliongeza kwa kusema kuwa sehemu ilipoamgukia ndegevita hiyo haikuleta madhara yeyote ya binadamu, nyumba wala miundombinu.

No comments:

Post a Comment