KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday 27 February 2015

MAUAJI YOHANA WABUNGE GEITA JITOKEZENI

WABUNGE wa Mkoa wa Geita wametupiwa lawama kutokana na kushindwa kujitokeza katika tukio la mauaji ya mtoto mwenye ulemavu wa ngozi (Albino), Yohana Bahati.
Tukio hilo la kusikitisha limetokea hivi karibuni ambapo baadaye mwili wa mtoto huyo aliyetekwa ukujakuepatikana ukiwa umekatwa miguu na mikono yote na kiwiliwili chake kufukiwa shambani katika kitongoji cha mapinduzi kijiji cha Rumasa ndani ya hifadhi ya msitu wa Biharamulo wilaya ya Chato mkoani Geita.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi katika maeneo ya Posta jijini Dar es Salaam, wakazi wa jiji hili, walisema ni jambo la aibu kwa bunge hao kukaa kimya kama vile hawanatarifa na kilichotokea.

Salome Julius, alisema kuwa kushindwa kwa wabunge hao kujitokeza kunadhihirisha ukweli kwamba mauaji ya Albino yanaratibiwa na wanasiasa wenye tama ya vyeo, wakishirikiana na waganga wasio jail uhai wa mwanadamu mwingine kutokana na tama ya fedha.

“Hadi leo hakuna hata mbunge mmoja ambaye amekwisha jitokeza na kuonesha kuwa kilichotokea hakiwahusu na wamenyamaza kimya,”alisema Salome.

Khadija Jumanne, alisema pamoja na mtoto kunyofolewa viungo vyake bado mama wa mtoto hyo, Ester Jonas alijeruhiwa kwa mapanga wakati akipigania maisha ya Yohana.

Alisema, hivi sasa Ester amelazwa lakini cha kushangaza hadi leo ikiwa zimepita zaidi ya wiki mbili hakuna hata Mbunge mmoja ambaye amekwenda kumjulia hali kitendo ambacho kinazidisha wasiwasi kwa wananchi kuamini kuwa kweli  wanasiasa ndio wanaoratibu unyama huo.

“Niwaombe wabunge wa Geita wakae chini chini na kisha wafikie uawamuzi wa busara wakwenda kumjulia hali Estera kitendo ambacho kitwajengea imani kwa wanachi,”alisema Khadija. 
 

Hivi karibuni Mtoto huyo wa mwaka mmoja alitekwa nyumbani akiwa amebebwa na mama yake mzazi, Esther ambaye alijeruhiwa katika tukio hilo kwa kupigwa panga usoni.

Kwa mujibu Kamanda wa polisi mkoa wa Geita, Joseph Konyo, mwili huo ulipatikana katika shamba la mahindi lisilo rasmi kutokana na kulimwa ndani ya hifadhi ya msitu wa Biharamulo wilayani Chato.

Kamanda SACP Joseph Konyo alisema maiti ya mtoto huyo iligunduliwa na mpita njia katika shamba la mahindi lililopo kitongoji cha tatu kutoka nyumbani kwao, baada ya kuona kipande cha nguo yenye damu ambapo alipiga yowe lililowakusanya wanakijiji ndipo walifukua shimo alipokuwa kafukiwa na kukutwa akiwa hana mikono na miguu yote.


Wakati huo huo hali ya mama Ester Jonas ambaye ni mama wa mtoto huyo bado ni tete na madaktari wa hospitali ya rufaa Bugando wanaendelea na juhudi za kuhakikisha hali yake inaimarika.

No comments:

Post a Comment