VIJANA
wanaodaiwa kuwa walitumwa na Mwalimu wa Shule ya Sekondari Kibasila, Gaudensia Albert,
aliyeishi na kinyesi kilichochanganyika na matapishi kwa muda wa miaka miwili, juzi
walikwenda kudai vyombo vilivyokuwa vimehifadhi uchafu huo.
Mrundikano
wa uchafu huo uliteketezwa juzi chini ya uangalizi mkali wa Jeshi la Polisi na maofisa
Afya wa Manispaa ya Temeke,
wakishirikiana na Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Kisiwani, Kata ya Sandari,
jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa mtaa huo, Yahya
Bwanga, alisema haelewi vijana hao ambao hakujua idadi yao walikuwa na lengo
gani.
Alisema
vijana hao walijitokeza juzi na kujitambulisha kuwa ni ndugu wa mwalimu huyo
na kwamba walitumwa kuchukua vyombo hivyo.
“Juzi
usiku walikuja vijana kwenye ofisi yetu ya serikali ya mtaa wakati mimi
sikuwepo, lakini walimkuta mjumbe akawahoji wakaonekana wamekuja kuchukua vile
vyombo vilivyokuwa na uchafu kwamba
walitumwa na yule dada.
“Kwa
kweli sisi tunashangaa kwa vijana hao kudai vyombo hivyo, kwani tulitarajia
kuwa wangeulizia kuhusu vyombo vile ambavyo vimebaki chumbani kwake, leo
wanauliza kuhusu vile vichafu, ni ajabu kwa kweli,” alisema Bwanga.
Bwanga
alisema vijana hao waliwafahamisha kuwa vyombo havikuwepo kwa vile kazi ya
kuteketeza uchafu huo ilifanywa na manispaa, hivyo kama walikuwa wakivihitaji
wanapaswa waende huko.
“Hapa
ndipo penye utata, juzi tumeambiwa kuwa yuko Muhimbili anapimwa akili, leo
tunaambiwa kuwa anadai vyombo vyake. Tumewaambia waende manispaa, kwani wale
ndio wanaojua kama vyombo vile kitaalamu vina maradhi au la, pia wameondoka
navyo,” alisema Bwanga.
Naye
Reuben Shayo, baba mwenye nyumba wa Gaudensia, alisema usalama wa vyombo vyake
upo kwa vile Diwani wa Sandari, Abel Tarimo, alinunua kufuli jipya kwa ajili ya
kufunga mlango wa chumba hicho chini ya ulinzi wa viongozi wa kata wakiongozwa
na Sajenti wa Polisi, Ramadhani Kagolo, huku funguo akikabidhiwa Mwenyekiti wa
Serikali ya Mtaa.
Hata
hivyo jitihada za kumpata mwalinu huyo zimegonga mwamba kutokana na simu yake
kuita muda mrefu bila kupokewa tangu lilipotokea tukio hilo.
Wakati
wa uteketezaji wa uchafu huo, Ofisa wa Afya wa Manispaa ya Temeke, Floyd Tembo,
alisema mwalimu huyo alikuwa amelazwa Muhimbili.
Tukio
hilo ambalo limewaacha wakazi wa eneo hilo na maswali mengi, lilitokea Februari
22 na kuteketezwa Jumatano Februari 25, mwaka huu.
No comments:
Post a Comment