KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday 1 March 2015

HONDOGO WAJIAANDAA KUTUMIA NGUVU YA UMMA

WAKAZI wa Kitongoji cha Tembo, Hondogo Kata ya Kibamba wilayani Kinondoni, wamesema wanatarajia kutumia nguvu ya umma kubomoa banda lililojengwa na kuziba barabara katika eneo hilo.
Mgogoro huo wa kuzibw barabara hiyo kunawafanya wakazi wa eneo hilo kupata tabu katika kujipatia huduma za kijamii upande wa pili.
Wakizungumza na SAUTI YA WALEMAVU.BLOG leo, wakazi hao walisema hawaelewe kuna kitu gani kinachowafanya viongozi wa kuanzia ngazi ya mtaa, Kata hadi Manspaa washindwe kumuondoa mvamizi huyo.
Kwa niaba yao, Ramadhan Mkude, alisema  wanatarajia kufanya hivyo kwa vile mgogoro huo umechukuwa muda mrefu, bila viongozi wa Manispaa hiyo kuchukuwa hatua ya kuumaliza japo wanaufahamu vizuri.
“Sasa acha tujipange kwa ajili ya kulibomoa wenyewe ili kuondoa usumbufu tunaoupata kutokana na kuzibwa barabara, hatupendi kutumia nguvu lakini wakati mwingine haki inawezekana ikaja kwa njia hii,”alisema Mkude.
Mkude, alisema mgogoro huo una zaidi ya miaka mitano sasa ambapo Mei 13, 2013, baadhi ya viongozi wa Idara ya Ardhi walitembelea eneo hilo ili kufanya uchunguzi wa mgogoro huo.
Alisema walichobaini katika ziara hiyo ni kwamba Ramani inaonesha kuwa barabara inayolalamikiwa inaupana wa mita kumi kutoka barabara itokayo Morogoro kuelekea Kibwegere.
Mkude alisema katika taarifa ya uchunguzi huo walibaini kuwa ni kweli kuna banda limejengwa kinyume cha sheria katika barabara hiyo, huku mmiliki akidai kuwa hilo ni eneo lake.
Alisema hata hivyo, katika taarifa hiyo wamejiridhisha kuwa mmiliki anayedai kuwa eneo hilo ni lake anaonesha kuwa mbishi kwani pamoja na kutakiwa na Baraza la Ardhi kufika katika kikao siku hiyo, alikaidi wito huo halali.
Mkude alisema baada ya uchunguzi huo Ofisi ya Mkurugenzi wa Maniaspaa hiyo ya Kinondoni, Oktoba 25, 2013, ili mwandkia barua Afisa Mtendaji Kata wa Kibamba,  barua hiyo ikisainiwa kwa niaba ya Mkurugenzi na Ofisa aliyeitwa Omary Mauya.

Alisema barua hiyo, ilisema kwa kuwa barabara hiyo iko chini ya Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni hivyo basi ikamuomba kupitia ofisi yake ya Kata afanye utaratibu wa kubomoa banda hilo ili barabara hiyo iweze kupitika na kuondoa usumbufu kwa wananchi hao.

Mkude, alisema lakini hadi leo banda hilo lipo, mmiliki wake anazidi  kero kwani wakati mwingine anaingilia miundombinu ya maji hivyo kuwafanya wananchi wataabike katika kupata huduma hiyo.

No comments:

Post a Comment