KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday 27 March 2015

ACT-TANZANIA CHA REKEBISHA KATIBA

Katibu Mkuu wa ACT, Mwigamba katikati ni Mwenyekiti wa chama hicho Mambo na mwanachama mwingine
CHAMA cha Uwazi na Mabadiliko (ACT-Tanzania), kimefanya marekebisho ya Katiba kwa kuingiza cheo kipya cha Kiongozi Mkuu wa chama ambaye atakuwa mwenye kauli ya mwisho kuhusu masuala yote ya chama.

Katibu Mkuu wa chama hicho, Samson Mwigamba alitoa kauli hiyo, wakati alipozungumza na wandishi wa habari kuhusu kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Alisema, wamefikia hiyo kwa vile nafasi hiyo haiko katiba katiba wanayo itumia sasa, baada ya kukamilika watatoa taarifa kwa wanachama wake wanaotaka kugombea nafasi hiyo katika uchaguzi unaofanyika leo.

“Nafasi nyingine zote za kitaifa yani Mwenyekiti Taifa, Makamu mwenyekiti wa Bara na Visiwani na wengine hizo ziko katikaKatiba ya Chama ambapo wagombea wengi tayari wamekwishakua fomu kwa ajili ya kugombea nafasi hizo,”alisema Mwigamba.

Mwigamba, alisema kiongozi huyo ndio atakuwa na fursa ya kugombea urais wakati wa Uchaguzi Mkuu kila utakapofika.

“Kuanzishwa kwa nafasi hii kutasaidia kumuepusha rais wan chi kuwa na kofia mbili bali awe kiongozi wa nchi tu,”

Mwigamba alifafanua kwa kusema kuwa baada ya agenda ya marekebisho hayo, kitiba hiyo itaanisha tofauti ya za utendaji wa kiongozi mkuu wa chama na mwenyekiti.

Aidha, mkutano huo ulitarajiwa pia kutoa taarifa za utendaji wa chama hicho tangu kilipoanza, kadhalika walifungua Kikao cha Halmashari Kuu.

Mwenyekiti wa chama hicho, Shaba Mambo, alisema wakati umefika sasa kwa chama hicho, kufanya uchaguzi ili kupata vuongozi wa kudumu kwani tangu kilipoanzishwa, hata baada ya kupata usajili wa kudumu kilikuwa kikiongozwa na viongozi wa muda.

Leo chama hicho, kitafanya uchaguzi wa viongozi wake wa ngazi zote ambapo kesho kitazinduliwa huyo  ikiwa ni ishiria kuwa kimeanza safari.

Uzinduzi huo utahudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kisiasa wa ndani na nje, pia na taasisi nyingingine.


No comments:

Post a Comment