KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Thursday 5 March 2015

DK. BILAL: HAKUNA ATAKAE KOSA MAFAO YAKE

Dk. Bilal, akizungumza na wandishi wa habari, wakati wa uzinduzi wa Kongamano la Mifuko ya Kijamii ambalo ni la siku mbili, likianzia leo na kumalizika kesho.

NA MWANDISHI WETU
MAKAMU wa Rais Dk. Mohammed Gharib Bilal, amesema serikali itahakikisha kila mstaafu analipwa mafao yake kutoka katika  Mifuko yao ya Hifadhi ya Jamii.
 
Bilal, alisema hayo jijini Dar es Salaam jana, wakati akizindua kongamano la siku mbili la wadau wa mifuko hiyo inayosimamiwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usalama wa Mifuko (SSRA).

Bilal alisema serikali inatambua kazi nzuri iliyofanywa na wastaafu ambao wengi wao walifanya kazi kwa uaminifu mkubwa na hatimaye kuchangia maendeleo nchini.

 “Mifuko hii tumeianzisha makusudi ili kuwalea wastaafu baada ya kuwa wamefanya kazi nzuri katika nchi yetu hivyo hawastahili kuachwa wahangaike,” alisema Dk. Bilal.

Aliwataka wasimamizi wa mifuko hiyo kutumia mkutano huo kama chachu itakayozidi kuwajengea uwezo wa kuelewa maeneo mbalimbali ya uwekezaji.

“Hivi sasa mifuko hii inawekeza kwa ajili ya kujitunisha na lengo kubwa ikilenga kuwasaidia wanachama wake katika masuala mbalimbali ya kijamii ikiwemo ajira,” alisema.

Naye Mkaguzi Mkuu wa Mifuko hiyo, Peter Mberwa alisema, hivi sasa wametoa muongozo utatumika kisheria na mifuko hiyo ikilinganishwa na awali ambapo walikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa sheria.

No comments:

Post a Comment