Kiongozi
wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, amesema jamii wakiwemo viongozi wanapaswa
kujifunza kwamba maisha ya duniani si ya kudumu, hivyo wanatakiwa kutenda wema
wakati wote.
Salamu za
Mbowe ambaye hata hivyo hakuweza kuhudhuria kutokana na kwamba yuko safarini
kikazi, zilitolewa kwa niaba yake na Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema),
Joshua Nassari, ambaye alisema wameguswa na msiba wa mbunge mwenzao.
“Nimesimama
hapa kutoa salamu za Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, ambaye yupo safarini
…lakini pia sisi na wabunge wenzetu wa upinzani tuko hapa kumsindikiza mbunge
mwenzetu katika safari yake ya mwisho, hivyo itikadi zetu tunaziweka pembeni.
“Katika
kipindi kama hiki ambacho akizoeleki, tunapaswa kujifunza kwamba maisha ya hapa
duniani si ya kudumu, hivyo tunapaswa kutenda mema ili tutakapoitwa tuwe salama
…na katika kufanya hivyo tuongozwe na Kitabu cha Biblia cha Zaburi kinachosema
‘Nitayainua macho yangu, nitazame milima…” alisema Nassari.
Miongoni
mwa viongozi na wabunge wa upinzani waliokuwapo katika Viwanja vya Karimjee
kumuaga Kapteni Komba ni pamoja na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa,
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, Mwenyekiti wa TLP, Augustino Mrema,
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi, Mbunge wa Mbozi Mashariki
(Chadema), David Silinde na Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Naomi Kaihula.
Salamu za CCM
Kwa
upande wake, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, alisema marehemu Komba
atakumbukwa na wengi kwa sababu alikuwa mfano wa kuigwa kwa Wana CCM, wanasiasa
na wasanii kutokana na mchango wake wa maneno na hamasa katika nyimbo zake.
Kinana
alisema alikuwa na kipaji cha pekee kutunga na kuimba nyimbo za CCM katika
chaguzi na za kitaifa, za furaha na huzuni, hata kuwatia moyo Watanzania katika
tukio hilo husika.
Kinana
alitoa mfano kwamba mwaka 1978 wakati wa vita ya kumng’oa Idd Amin katika ardhi
ya Tanzania, marehemu Komba aliwatia hamasa wanajeshi wenzake kwa kuhamasisha
kwa nyimbo mbalimbali katika mapambano.
“Si kwa tukio la vita ya Idd Amin tu, Komba
aliimba wakati wa msiba wa Mwalimu Julius Nyerere, marehemu Komba atakumbukwa
sana na wengi kwa sababu alikuwa ndugu, rafiki, mwalimu, mwanajeshi,
mwanasiasa, mtumishi hodari na mzalendo kwa taifa lake.
“CCM
tutamuenzi marehemu Komba kwa mengi aliyoyafanya katika chama na taifa
…ametangulia nasi tutafuata kwa sababu kifo hakikwepeki, chama kinatoa salamu
za rambi rambi kwa Bunge, Serikali na sh. milioni tano kwa familia kufuatia
msiba huu mzito,” alisema Kinana.
No comments:
Post a Comment