KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday 3 March 2015

JESHI LA POLISI PWANI LAKAMATI WAMIAJI SITA






JESHI la Polisi mkoani Pwani linawashikilia watu sita raia wa Malawi kwa kosa la kuingia nchini bila kibali.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Kamishina Mwandamizi (SACP) Ulrich Matei alisema watu hao walikamatwa juzi eneo la mizani ya Maili moja Kibaha kutoka Zambia kwenda Dar es salam.

Kamanda Matei alisema kuwa katika tukio hilo raia hao wa Malawi walikua wakisafiria gari lenye namba za usajili BQ7828 aina ya Mitsubishi Fuso iliyokua ikitokea Zambia kwenda Dar es salam usiku wa kuamkia Machi 03.

Waliokamatwa katika tukio hilo ni Saam Manda(19), Meshack Nigata(22), Juniour Mngonje(26), Isack Ndamba (20), Weziel Longwe (21) na Mource Zawinja(35).
Kamanda Matei alisema watuhumiwa hao watakabidhiwa idara ya uhamiaji na hatua za kisheria dhidi yao zitachukuliwa.

Wakati huo huo, watu wawili wamepoteza maisha katika ajali ya barabarani iliyotokea juzi majira ya saa 11 jioni huko Ndagoni kata ya Baleni Wilaya ya Mafia.

Katika tukio hilo gari lenye namba za usajili T842 ASC aina ya Mitsubish Fuso ikiendeshwa na Salehe Yahaya iliacha njia na kupinduka .

Kamanda Matei amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja waliopoteza maisha kuwa ni pamoja Deodatus Sapila (21) na Said Simba (25).

Tukio jingine katika Wilaya ya Bagamoyo, Kombo Zuberi (18) ambaye ni mvuvi amekutwa akiwa amefariki dunia chooni huku mwili wake ukiwa na alama za kujidunga sindano kwenye kiwiko cha mkono wa kulia.

Taarifa ya tukio hilo inabainisha kuwa kando ya mwili wa marehemu ilikutwa bomba la sindano lenye dawa za kulevya na pakti ndogo ya dawa hizo.

No comments:

Post a Comment