MKURUGENZI wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Agnes Kijazi, amewataka wakazi wa maeneo ya Ziwa Victoria kuchukuwa tahadhari kutokana na mvua kubwa zinaotarajiwa kunyesha kuanzia sasa kuwa huenda zikasababisha hatari ya mafuriko.
Mkurugenzi huyo alikuwa akitoa muelekeo wa
mvua za masika zinazotarajiwa kunyesha kuanzia Machi, Aprili na Mei mwaka huu
jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na wandishi wa habari huku
akiambatana na wadau wa Kilimo na Afya, Kijazi, alisema izingatiwe kuwa pamoja
na kuwapo kwa uwezekano wa matukio ya mvua kubwa katika maeneo yanayotarajiwa
kupata mvua juu ya wastani, hali hiyo pia inaweza kujitokeza katika maeneo
ambayo yanatarajiwa kupata mvua za wastani hadi wa chini.
Alitaja maeneo hayo kuwa ni mikoa ya
Kagera, Mara, Mwanza, Geita hata hivyo kuna baadhi ya maeneo ya mikoa hiyo pamoja na Simiyu, Shinyanga vipindi
vya mvua hizo zilikwishaanza tangu Februari mwaka huu, zinatarajiwa kuwa za wastani hadi juu ya
wastani.
‘Msimu wa mvua unarajiwa kuanza mapema
katika maeneo ya kanda ya ziwa Victoroa na baadhi ya maeneo ya ukanda wa Pwani
ya Kaskazini,”alisema Agnes.
Adha, Alisema katika maeneo yanayopata
misimu miwili ya mvua, msimu huo wa masika utaanza Machi hadi Mei ambapo
itakuwa ni mahususi katika maeneo ya nyanda za juu kaskazini mashariki mwa
mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara.
Vilevile katika Pawani ya kaskazini mwa
mikoa ya Dar es Salaam Tanga, Pwani, Morogoro-kaskazini pamoja na Visiwa vya
Unguja, Pemba na mikoa ya Kanda ya Ziwa victoria.
“Mvua za wastani hadi juu ya wastani
tunazitarajia katika baadhi ya maeneo hususan kanda ya ziwa victoria na maeneo
ya kusini ya nchi, hata hivyo, hali ya mvua haitakuwa ya kuridhisha katika
maeneo mengi ya nchi,”alisema Agines.
Akizungumzia mifumo ya hali ya hewa, Agnes,
alisema katika kipindi cha Machi hadi Mei mwaka huu kunatarajiwa kuwa na
ongezeko la joto la bahari katika eneo la Tropikali kati ya Bahari Pasifiki.
Alisema hali hiyo ya jotola juu ya wastani
linatarajiwa katika ukanda wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi (Pwani ya Afrika
Mashariki) na Mashariki mwa Bahari ya Hindi (Indonesia).
Agnes alisema hali hiyo itasababisha upepo
kutoka mashariki utakaombatana na unyevunyevu hafifu wa hewa yenye unyevunyevu
kutoka katika misitu ya Kongo kuelekea maeneo ya magharibi mwa nchi, mikoa ya
kanda ya kati kuna nyanda za juu kusini-magaribi na hivyo kusababisha upungufu
wa mvua katika maeneo hayo.
Mkurugenzi
wa Usalama wa Chakula, Karim Mtambo, alisema kutokana na utabiri huo anawashauri
wakulima wa maeneo ya Kanda ya ziwa Victoria kuandaa mashamba na pembejeo
mapema na kuzingatia ushauri wa wataalam wa kilimo kwa matumizi sahihi ya ardhi
na mbegu.
“Katika baadhi ya maeneo ya nchi hususan
kanda ya ziwa Victoria nyanda za juu kusini magharibi na maeneo ya mkoa wa Mtwara
hali ya unyevunyevu wa udongo, tunautarajia kuwa ya utatosheleza katika
shughuli za kilimo,”alisema Mtambo.
Mtaalam wa Afya, kutoka Wizara ya Afya na
Ustawi wa Jamii, Jubilata Bernad, alisema katika kipindi hicho cha mvua,
menejimenti ya maafa na wadau wengine wanashauriwa kuchukua hatua stahiki
katika utunzaji wa mazingira, upatikanaji wa majisafi na salama na usambazaji
wa dawa, maji na chakula ikiwa ni hatua za
kujiandaa na kukabiliana majanga yanayoweza kutokea.
No comments:
Post a Comment