Katibu Mkuu wa zamani CCM,Yusuf Makamba akilia baada ya kutoa heshima za mwisho wakati wa kuaga mwili wa Kapteni Komba. Na Mwandishi Wetu |
KATIBU
Mkuu wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rajabu Yusufu Makamba amesema hadi
sasa anamfahamu Rais wa nchi hii hajae.
Makamba
alisema hayo juzi wakati alipokuwa kwenye shughuli ya kuuaga mwili wa maerehemu
Kepteni John Komba, ambaye alifariki Februari 28 mwaka huu baada ya kusumbuliwa
na ugonjwa wa kisukari.
Makamba
alikuwa akijibu swali la mwandishi wa habari aliyekuwa akitaka kujua kama
msimamo wake kisisasa na marehemu Kepteni Komba ilikuwa ikifanana kuhusu urais
katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Alisema
haikuwa sahihi kuzungumzia suala hilo katika eneo lile la viwanja Karimjee, kwa
vile walikuwa pale kwa ajili ya maombolezi ya msiba Kepteni Komba ambaye pia
alikuwa Mbunge wa Mbinga Magharibi.
“Sikuja
kuzungumza masuala ya uchaguzi tuko hapa kwa ajili ya msiba hivyo niacheni
katika hilo,”alisema Makamba.
Hata
hivyo, Makamba alisema kama kuna mwandishi anataka kujuaRais ajaye basi ni vema
akamtafuta wakati mwingine tena akimfuata nyumbani kwake.
Katibu
huyo, Mkuu wa zamani, alijigamba kuwa hadi sasa anamfahamu Rais wan chi hii
ajae, lakini bila ya kufafanua.
“Rais
ajae mimi na mfahamu kama nilivyokwambia ukitaka kumjua njoo nyumbani kwangu Tegeta
tutazungumza na nitakuambia,”alisema Makamba.
No comments:
Post a Comment