KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Wednesday 4 March 2015

WATU 38 WAFRIKI DUNIA SHINYANGA KWA MAFURIKO

Mwenyekiti wa CCM, mkoani Shinyanga, Mgeja
OFISI ya Waziri Mkuu imesema katika hatua za awali imetoa msaada wa kuwakoa watu waliokumbwa na mafuriko yiliyosababishwa na mvua iliyoambatana na upepo mkali, aliyotokea juzi katika Kata Mwakata wilayani Kahama mkoani Shinyanga.


Akizungumza na Blog  jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Maafa, Naima Mrisho, alisema hadi sasa kitengo hicho tayari kimekwishachukua hatua za dharura.

Alisema linapotokea tukio kama hilo hatua wanazochukuwa ni kuwaokoa majeruhi ambao wamebaki katika eneo la maafa.
Alisema kitengo hicho tayari kimeshatoa msaada wa vyakula na mahema kwa ajili ya kuwahifadhi baadhi ya familia ambazo makazi yao yamebomolewa na mvua hiyo.

“Tunawasiliana na wadau wengine ili wasaidie watu hao walipatwa na maafa hayo yaliyotokana na mvua kubwa. Pia ofisi inajipanga zaidi,” alisema Naima.

Mgeja atoa pole
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, aliwapa pole wale wote waliokumbwa na maafa hayo, huku akiwataka wawe na subira.

“Mimi natokea safarini kwenye msiba wa Kepteni John Komba lakini kikubwa ni kuwapa pole wote walioathirika na janga hilo, kwa kweli ni lakusikitisha,” alisema Mgeja.


Alisema wanaishukuru serikali kwani iliweza kufika haraka katika tukio hilo, ambapo pia waliyaomba mashirika mbalimbali kufika hapo kwa lengo la kujitolea msaada.

Alisema serikali iko pamoja na wananchi na kila jitihada zinafanyika ili iweze kuwasidia wananchi hao.

No comments:

Post a Comment