VURUGU zimezuka leo eneo la Fire wilayani Ilala, Dar es Salaam, baada madereva wa bodaboda kuwataka
askari polisi kumpeleka hospitali mwenzao aliyeumia mguu kutokana na kipigo cha
askari hao.
Askari hao
wanadai kuwa walikuwa wakitekeleza tamko la serikali la kuwataka madereva wa
bodaboda na bajaj kutoingia katikati ya jiji.
Machi
mwaka 2009, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilifanya marekebisho
katika Sheria ya Leseni za Usafirishaji ya Mwaka 1973 ambapo pikipiki za
kawaida na za magurudumu matatu maarufu kama Bajaj kwamba zimeruhusiwa kuwa
moja ya vyombo vya usafiri vilivyoruhusiwa kutoa huduma ya kubeba abiria kwa
malipo au kukodi.
Baada ya marekebisho ya Sheria
hiyo, Mamlaka ya Usafiri wa Majini na nchi Kavu (Sumatra) ilitengeneza kanuni
mpya kwa ajili ya utekelezaji zilizojulikana kama "The Transport Licensing
(Motor cycles and Tricycles) Regulations, 2010.
Akizungumza
na wandishi wa habari jijini leo, James Christopher, ambaye alikuwa ni miongoni
mwa mashuhuda wa vurugu hizo, alisema chanzo cha vurugu hizo ni uonevu wa
polisi hao wa wanaofanya doria kwa kutumia pikipiki ‘Tigo’.
“Tatizo
limekuja baada ya dereva wa bodaboda kupigwa na askari, kuachwa akiwa ameanguka
ndani ya mtaro wenye maji machafu kule Jangwani, wenzake walipoona hivyo, walimwinua
kutoka kule na kumleta hapa Fire na
kuwabwagia askari hao wampeleke hospitali, ambapo walidai kuwa amevunjika mguu
lakini mimi sikuona jinsi alivyovunjika,” alisema Christopher.
Alisema,
baada ya kumfikisha kwa askari hao yalizuka mabishano kati yao na madereva wa
bodaboda ambao walikuwa wakilazimisha mwenzao apelekwe hospitali kwa vile
askari hao walimuumiza na kumtelekeza.
Christopher,
alisema inavyonekana askari hao hawakupendezwa na hatua hiyo, hali iliyowafanya
waanze kuwafukuza madereva hao wa bodaboda.
Aliongeza
kwa kusema kuwa kitendo hicho kiliongeza hasira kwa madereva wa bodaboda ambao walikuwa
wakiongezeka, huku wakijibu kwa kuwarushia mawe askari.
Christopher,
alisema baada askari kuona hali inazidi kuwa mbaya iliwabidi wanze kufyatua
risasi za moto hewani huku madereva na askari hao wakikimbia hovyo.
“Hali
ilikuwa inatisha, unaambiwa hata trafiki aliyekuwa akiongoza magari pale Fire
alikimbia kwa ajili ya kupata msaada kwa wenzake,” alisema Christopher.
Alisema
wakati vurugu hizo zikiendelea madereva hao wa bodaboda wakalipiga mawe gari la
serikali namba STL 156 ambalo wandishi walilishudia ilikiwa Kituo cha
Polisi Msimbazi.
Shuhuda
huyo, alisema baada ya purukushani hizo polisi waliondoka na dereva wa bodaboda
aliyeumia ambapo haikufahamika mara moja kuwa wamempeleka wapi.
Hata
hivyo, baada ya askari hao kuondoka, muda mfupi zilifika gari nne za polisi zikiwa
zimewabeba baadhi ya viongozi wa polisi hao ambao walionekana kuorodhesha majina
ya askari ambao walianzisha mabishano na madereva hao wa bodaboda.
Alipotafutwa
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (ACP), Lucas
Mkondya, ili kutoa ufafanuzi juu ya tukio hilo alijibu kwa ufupi kuwa atatoa
taarifa siku ya kutoa taarifa.
“Tutawaambia
lakini kwa sasa hivi sijapata kitu cha kuaambia, tutakapokamilisha
tutawaambia,” alisema Kamanda Mkondya.
No comments:
Post a Comment