KATIBU wa shirika la Dawa Asili na Ulinzi wa Mazingira
nchini Bonivetura Mwalongo ameunga mkono Tamko la Serikali la kutaka kufuta
usajili wa baadhi ya Taasisi na Mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo
yalisajiliwa kuazia mwaka 1954 hadi 2013 kutokana na kushindwa kufuata sheria
na masharti ya usajili.
Akizungumza Ofisini kwake Dar es Salaam jana mbele ya
waandishi wa habari waliofika ofisini hapo kutaka kujua kwanini Chama cha
Watatibu wa Tiba Asili Tanzania (ATME) kimefutwa rasim na kuazishwa kwa Chama
kingine cha Shirika la Dawa Asili na Ulinzi wa mazingira.
Mwalongo alisema kuwa Chama hicho kilipoteza sifa za kuendelea
kuwa uhai ,hivyo kufa kwake kumekwenda sambamba na Tamko la Serikali la kutaka
kufuata taasisi na mshirika yote ambayo yamepoteza sifa na masharti ya
usajili wake,hivyo hata ATME ilipoteza sifa hizo.
Alisema kuwa lazima ifike wakati watanzania waache kuchochea hata
mambo ambayo yapo kisheria badala yake waisaidie Serikali katika kusimamia
sheria ziliwekwa,hivyo hata viongozi wadini wanatakiwa kuwa mstari wa mbele
katika kuhakikisha watu hawavunji sheria na si wao kuwa sehemu ya walalamikaji.
Alisema kuwa viongozi wa dini wao ni dira katika nchi, hivyo
hategemei kuona kunajitokeza hali yeyote ya vurugu na lazima ielewekwe kwamba
viongozi hao wanamchango mkubwa katika taifa hivyo anaamini Serikali haitatumia
mabavu katika hilo
bali kila jambo litafuata sheria zilizowekwa.
“Lazima sheria ifuatwe kwani hatuwezi kuwa na taifa ambalo watu
wake hawafuati sheria zilizokwa ,hivyo naunga mkono tamko hilo la Serikali na kamwe lisitafasiliwe
vibaya na hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu,”alisema Mwalongo.
Aliongeza kuwa tatizo kubwa lililopo hivi sasa katika nchi yetu
watanzania wanapenda kuchanganyika mambo ya kisheria na siasa hivyo lazima
siasa ikae mbali na hasa linapokuja suala la kisheria.
Katika hatua nyingine akizungumzia shirika hilo jipya alisema kuwa alisema kuwa lipo kwa
ajili ya kuendelea kufanya kazi ya kusimamia wadau wa Dawa za Asili nchini ili
waweze kufanya kazi kwa kufuata miongozo mbalimbali kwa mujibu wa sheria
zilizokwa.
Mapema mwezi huu Serikali kupitia Wizara ya mambo ya ndani ya nchi
ili tangaza kufuata taasisi na mashirika yote ikiwamo taasisi za dini
baada ya kubainika kuvunja sheria ikiwemo kushindwa kupeleka taariza za ukaguzi
wa hesabu zao katika kila mwaka.
No comments:
Post a Comment