JESHI la Polisi Kanda
Maalumu ya Dar es Salaam limesema litarekebisha kituo cha Polisi cha Kimara
kilichopo Kata ya Saranga, wilayani Kinondoni ili kiweze kufanya kazi saa 24.
Akizungumza jijini Dar
es Salaam juzi, Kamanda wa Kanda
Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova,
alisema maboresho hayo yanatokana na wingi wa wakazi wa eneno hilo.
Alisema mbali na kituo
hicho kufanyiwa marekebisho, vituo vingine navyo vitafanyiwa marekebisho, ili viweze kuhudumia
wananchi muda wote.
“Tunajipanga kuboresha vituo vya polisi
ambavyo kwa sasa vinafungwa kuanzia saa 12 jioni na kufunguliwa saa 12 asubuhi,”
alisema Kamanda Kova.
Alisema Jeshi la Polisi
halijachoka kuwasaka watu wanaosadikiwa
kuwa ni majambazi ambao wanavamia
vituo vya polisi na kusababisha mauaji
huku wakichukua silaha.
Aliongeza kuwa kazi ya
Jeshi la Polisi ni kupambana na wahalifu wanaosumbua raia na kuwafanya waishi kwa hofu.
Kamanda Kova alieleza
jeshi hilo linaendelea na uchunguzi na kuwaomba wananchi watoe ushirikiano wa
kutosha kuwafichua wahalifu, ili kuendeleza amani nchini.
“Tukiwakamata tutawahoji kwa nini wavamie vituo vya polisi na kuchukua
silaha, wanazipeleka wapi wakati ni watu wa kawaida,” alieleza Kamanda Kova.
No comments:
Post a Comment