KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday 31 May 2015

BENET GROUP & MICROFINANCE LTD YAKOPESHA VIJANA 22 BODABODA



VIJANA 22 wanaofanyabiashara ya kusafirisha abiria kwa kutumia pikipiki (bodaaboda), wameweza kumiliki pikipiki baada ya kuthubutu kuchukua mkopo wenye riba nafuu wa vyombo hivyo kutoka kampuni Benet Group & Microfinance Ltd.
Vijana hao walifikia hatua hiyo baada ya kubaini kuwa pikipiki walizokuwa wakifanyaia kazi huku zikiwa sio mali yao zilikuwa zikiwarudisha nyuma kimaendeleo kwani hesabu waliyotakiwa kupeleka kwa mmiliki ilikuwa haiendani kipato wanachopata kwa siku.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Mtemi Mahungucillo, alisema Benet Group& Microfinance Ltd imechukua dhamana katika Kampuni ya Fekon ya China, ili iwawezeshe vijana kwa kuwapatia pikipiki hizo kwa mkopo wenye riba nafuu ukilinganisha na kwingine.
Alisema lengola kutoa mikopo hiyo kwa vijana ina lenga kuwawezesha vijana kujiari pia kumfanya kijana huyo aweze kumiliki pikipiki yake.
“Jumla ya mkopo huo wa pikipiki ni sh. milioni 2,356,000 ambao mkopaji atawajibika kuulipa ndani ya miezi nane kwa kulipa ama kwa kila wiki sh. 58,000 au kwa mwezi sh 232,000,”alisema Mahungucillo.
Mahungucillo, alisema kampuni hiyo inatoa fursa hiyo kwa mtu mbinafsi, kikundi, taasisi ya chama, dini na vikundi vya walemavu, vyote hivyo viewe vimesajiliwa kisheria.
Hata hivyo, mkurugenzi huyo alisema fursa hiyo inatolewa kwa wakazi wa jijini Dar es Salaam na Pwani.
Akizungumzia mkopo huo, Mohamed Mzuki, alisema anashukuru kupata pikipiki hiyo, kwa vile yeye ni mkulima huko Ifakara mkoani Morogoro anaamini itamsaidia katika shughuli zake za kilimo kama vile kubebea pembejeo na mazao wakati wa kuyarudisha nyumbani.
Naye Juma Kilangilo, ambaye ni dereva wa bodaboda maeneo ya Mabibo, alisema mwanzo alikuwa akiendesha ya mtu ambayo ilikuwa aikimbana katika malipo ya siku, lakini naamini kwa kupata yake anaamini itamkwamua katika matatizo yake ya uchumi na kumletea maendeleo kwenye familia yake.


No comments:

Post a Comment