KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday 31 May 2015

WATANZANIA WATAHADHARISHWA KUHUSU BAJETI YA MWAKA WA FEDHA 2015/16


MKURUGENZI Mtendaji wa Sikika, Irinei Kiria amewatahadharisha Watanzania kuwa wajiandae na kiama endapo Bunge litaridhia kupitisha bajeti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ya sh bilioni. 37 katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2015/16.
Kiria alisema hivyo, baada ya kubaini katika kipndi cha miaka mine iliyopita, bajeti ya dawa muhimu na vifaatiba imekuwa ikishuka na kusababisha ongezeko kubwa la uhaba wa dawa muhimu huku waathirika wakuu wakiwa wananchi wa hali chini.
Mkurugenzi huyo, alitoa kauli hiyo jijini Dare es Salaam jana, wakati alipozungumza na wandishi wa habari kwa kuitaka serikali iongeze Bajeti ya Dawa Muhimu na Vifaatiba kwa mwaka 2015/16.
“Kwa mwaka wa fedha 2015/16 bajeti imeshuka kwa kiasi kikubwa sana ikilinganishwa na mahitaji ambayo ni zaidi ya bilioni 500 ilihali bajeti iliyotengwa ni bilioni 37 tu,”alisema Kiria
Kiria, alisema ili kuepukana na tatizo hilo la uhaba wa dawa, taasisi hiyo inapendekeza serikali iongeze fedha zakutosha kwa ajili ya dawa muhimu na vifaatiba katika mwaka huo.
Alisema ongezeko hilo, litahakikisha upatikanaji wa dawanchini unaongezeka kufikia asilimia 80 katika mwaka 2016 kama inavyotarajiwa na mpango wa matokeo Makubwa Sasa (BRN).
Aidha, alisema kuwa serikali kupitia wizara za fedha na afya zinapaswa kuhakikisha fedha zilizotengwa kwa ajili ya dawa muhimu na vifaatiba zinatolewa kwa wakati ili kupunguza uhaba wa dawa nchini.
Vilevile alisema Wizara ya Afya itoe mwongozo na mikakati inayoeleweka na kuwezekana katika kutumia mapato ya afya ya halmashauri kwa ajili ya ununuzi wa dawa muhimu na vifaatiba.
Kiria, alisema kuwa pia ni vyema miongozo hiyo ikaweka wazi mifumo ya uwazi na uwajibikaji.
“Tunaelewa kwamba Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inapanga kutumia mapato ya mbadala/fedha za uchangiaji katika kusaidia bajeti ya dawa muhimu na vifaatiba katika mwaka wa fedha 205/16.
“Kwa kutumia fedha hizi ili kuziba pengo ni kitu kisichowezekana kwa sasa kwa sababu makusanyo na matumizi ya fedha hizi hazijulikani na hakuna taarifa kuwa ni kwa kiasi gani fedha hizi zinaweza kuziba pengo la upungufu wa Bajeti,”alisema Kiria.
Akizungumzia kushuka kwa bajeti hiyo katika kipindi cha miaka minne, Kiria, alisema mahitaji yamekuwa yakiongezeka huku bajeti ikishuka, mathalani mahitaji ya dawa muhimu na vifaatiba yameongezeka kutoka sh. bilioni 188 (2011/12), hadi sh. bilioni 577 (2014/15).
Kiria, alisema bajeti hiyo inayopangwa imepungua kutoka sh. bilioni 123.6 (2011/12), hadi  bilioni 70.5 kwa mwaka wa fedha wa 2014/15.
Alisema licha ya kupungua kwa fedha zilizotengwa, serikali imeakuwa ikitoa fedha hizo pungufu ya zile ilizoahidi.
Mfano mwaka 2011/12), iliahidi sh. bilioni 123.6 lakini ikatoa bilioni 98 tu na mwaka wa fedha (2014/2015), iliahidi 70.5 hadi sasa imetoa sh. bilioni 33.3.


No comments:

Post a Comment