KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday 24 May 2015

KAULI YA KIKWETE YAWAPENDEZA BAADHI YA WANACHAMA


KAULI ya Mwenyekiti wa Chama Mapinduzi (CCM), Rais ya Jakaya Kikwete, ya kukitaka chama chake kuteua wagombea wanaokubalika kwa watu na kwamba zama za kutegemea jina la chama kuwa zimepitwa na wakati, zimeungwa mkono na baadhi ya makada wa chama hicho.
Rais Kikwete alitoa kauli hiyo juzi wakati  akifungua Mkutano wa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM mjini Dodoma.
Wakizungumza na wandishi, kwa nyakati tofauti leo, makada wa chama hicho, Hamis Mgeja na Mgana Msindai, walisema, kauli hiyo inaonesha ni jinsi gani ndani ya CCM kuna ukomavu wa kisiasa.
Msindai, alisema hivyo kwa kuwa kauli ya Rais inaondoa mawazo yaliyojengeka vichwani mwa baadhi ya makada kwamba kiongozi mzuri ni yule anayekubalika kwa viongozi wa chama hicho.“Kauli ya Rais siyo mbaya kwa sababu amesema achaguliwe mgombea anayekubalika na watu, hapo sina tatizo, kiongozi anayekuabalika na watu kwa mfano katika makada wote waliojitokeza kugombea, tayari watu wanaye mtu anayekubalika hivyo sio vyema wakachaguliwa mgombea viongozi wa chama,”alisema Msindai.
Msindai, alisema kiongozi anayefaa kwa wakati wa sasa ni yule amabye anao uwezo wa kutoa uwamuzi ambao unalenga kukigeuza chama na kukirudisha kwanye mstari na kuijenga Tanzania yenye maendeleo yanayogusa wananchi wote.
Khamis Mgeja, alisema kauli hiyo imewapa faraja, kwamba mwenyekiti wao amekuwa ni mwuelewa na amewatangulia kusoma alama za nyakati.
“Kauli ambazo zinaonesha ndani ya CCM kuna ukomavu wa mtazamo na kwa kweli kiongozi atakaye kipa chama ushindi ni yule anayekubalika na wananchi na wala sio matakwa ya viongozi,”alisema  Mgeja.
Mgeja, alisema anaimani kuwa kauili hiyo ni njema kwani wamekuwa wakilizungumza kwa muda mrefu kwamba kiongozi wa kweli atatokana na matakwa ya wananchi hilo kwa muda mrefu sasa.
Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho, Yusuf Makamba, alisema inakuwa ni vigumu kwake kutoa maoni yake kuhusu kauli iliyotolewa na Mwenyekiti wake.
“Hayo ni maneno ya mwenyekiti unataka niseme nini yangekuwa yamesemwa na mtu mwingine ungeniuliza maoni yangu lakini mwenyekiti? Sina la kusema elewa masuala ya siasa nimestaafu, sasa nimekuwa mfugaji njoo une ng’ombe wangu mmoja anaitwa Madale amjifungua narudia hayo mambo nimestaafu.
Alisema mambo ya siasa hivi sasa amewaachia wanasiasa kama vile Januari Makamba hao ndio wanaoweza kuzungumzia siasa, akibainisha kwamba aulizwe maswali yanayohusu ufugaji.
Juzi mjini Dodoma, Rais Kikwete alisema zama za kushinda kwa mazoea kwamba mgombea akishateuliwa na CCM lazima ashinde, zimepitwa na wakati.
“Tusijidanganye kwamba anayeteuliwa ni lazima ashinde, tutateua mgombea anayekubalika na wengi, vinginevyo tutaula wa chuya,”alisema Kikwete.

Hata hivyo, Rais Kikwete alisema katika kufanya uteuzi, lazima wazingatie masilahi ya chama kwanza, mtu baadaye.

No comments:

Post a Comment