KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday 24 May 2015

MWENYEKITI WA UWAWADA, KIDUMKE: HAKUNA MAANDAMANO



WAFANYABIASHARA wenye ulemavu wa Soko la Mchikichini, Karume wilayani Ilala, jijini Dar es Salaam wamesema hawana mpango wa kuandamana tena kama walivyofanya siku tano zilizopita.
Wafanyabiashara hao Mei 21mwaka huu walifunga makutano ya barabara ya Uhuru na Kawawa wakipinga kitendo cha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ilala kuwatuma polisi na mgambo wa jiji kwenda kuvunja meza za kupangia biashara zao kwa madai kuwa eneo hilo sio rasmi wakati akijua fika kuwa walipewa kwa maandishi mbele ya mwanasheria wa halmashauri hiyo.
Kitendo cha askari hao kinadaiwa kuwa kilisababisha upotevu wa mali za wafanyabiashara hao kwa vile kazi hiyo ilifanyika kinyemela majira ya saa nne usiku bila ya wafanyabiashara hao kuelezwa kama kungefanyika zoezi hilo.
Akizungumza na wandishi wa habari leo,  Mwenyekiti wa Umoja wa Walemavu Dar es Salaam (Uwawada), Mohamed Kidumke, alisema, hakuna maandamano na kwa kawaida hata wanapotaka kuandamana hawana utaratibu wa kutoa taarifa bali wanashtukiza tu.
Alisema, hivyo kwa vile hivi sasa wako katika mazungumzo na serikali ya kuwapatia eneo la kudumu ili kuepuka mivutano ya mara kwa mara kati yao na serikali.
“Ijumaa tulikuwa na kikao na Mkurugenzi, Mkuu wa Wialaya, Ofisa maendeleo na Jamii kwa ajili ya kujipanga hasa kwa ajili mambo ambayo tuliyokuwa tukiya lalamikia lakini kubwa ilikuw ni kuweka mikakati ya kutafuta eneo la kudumu ili kuondoa usumbufu ambao unaonekana kujirudia rudia,”alisema Kidumke.
Alisema katika kikao hicho, walipendekeza kupewa eneo ambalo ni zuri na linawafaa kwa kuendesha shughuli zao, akibainisha kwamba wakipewa eneo hilo basi anaamini tatizo hilo litakuwa limekwisha.
“Hatuwezi kulitaja kwa sababu hivi  sasa tuko katika majadiliano kuhusu eneo hilo lakini yote hayo tumewaachia viongozi wa wilaya kwani wao ndio wenye wajibu wakutupatia eneo hilo,”alisema Kidumke.
Kidumke, alisema majadiliano yanaendelea leo kwa ajili ya kukukamilisha baadhi ya makubaliano ambayo yatakuwa kwa maadishi ili yaweze kufanyiwa kazi haraka.
Kuhusu uhalibifu wa mali na kuibiwa bidhaa zao, juzi, Kidumke, alisema kuwa mchakato wa kufanya tathimini unaendelea na kuahidi kuwa haki itatendeka hivyo kuwataka wenzake kuwa watulivu.
Aliongeza kwa kusema kuwa hivi sasa wafanyabiashara hao wameruhusiwa kuendelea na shughuli zao hadi hapo watakapopatiwa eneo la kudumu na kwamba hakuna atakayewabugudhi tena.
MWISHO   

No comments:

Post a Comment