KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday 29 May 2015

WANACHAMA WA CCM WATAKIWA KUFUATA TARATIBU NA KANUNI

Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam, Madabida

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida, amewataka wanachama wenye nia ya kuwania nafasi kama vile ubunge na udiwani kufuata kanuni na utaratibu wa chama.
Madabida, alitoa kauli hiyo baada ya kutakiwa kutoa ufafanuzi kuhusu madai kwamba diwani wa Kata ya Kijichi Anderson Charles amekuwa akijihusisha katika kumpitisha pitisha mmoja wa makada ambaye hivi sasa ni Mbunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika Jimbo la Kigamboni ambalo liko chini ya Faustine Ndugulile.
Akizungumza jijini leo, Madabida, kwanza alimtaka mwandishi amueleze alikozipata taarifa hizo.
Alisema licha ya kuwataka wanachama hao kufuta taratibu pia aliwashauri wote wenye taarifa amabazo hazina mashaka kuhusu wanachama wanaovunja taratibu na kanuni za chama kwa kujipitishapitisha kwenye majimbo yenye wabunge wa chama hicho, kuwafanya wakose raha na kushindwa kutekeleza ahadi zao wazifikishe wakiwataja wanaofanya hivyo.
Madabida, alisema chama hakitakuwa tayari kuzifanyiakazi taarifa za madai kama hayo, ambazo hazitaji chanzo halisi kwa vile zinaonekana kuwa ni za majungu.
Naye diwani wa Kijichi, Charles, alisema taarifa hizo ni za uzushi kwani kama zingekuwa za kweli basi kutokana na utaratibu wa chama chake anaamini kuwa angefikishwa kwenye Kamati ya Maadililakini kwa kuwa ni za uongo ndio maana hajafikishwa kwenye kamati hiyo.
“Wewe umeambiwa na mbunge mwenyewe, kama hajakuambia ni uongo na hizo ni za kwako wewe, na amini,”alisema Charles.
Aidha, alishangazwa na kauli kwmba anamsaidia mbunge huyo wa Afrika Mashariki kwa makubaliano kuwa akifanikiwa kuupata ubunge wajimbo hilo basi atamsaidia kupata umeya, jambo alisema ili uwe meya ni lazima kwanza upate udiwani.
“Tuhuma hizi ni za kitoto kwa mtu anayejua ni kwamba mbunge hana uwezo wa kumpa diwani umea isitoshe mimi nilikuwa meneja wa kampeni wa mbunge wa Kigamboni,”alisema.
Awali, taarifa hizo zilitolewa na baadhi ya wanachama watiifu kwamba mbunge huyo ambaye kwa sasa yuko nje ya nchi kwamba diwani huyo amekuwa mstari wa mbele kuona mbunge wao anakosa nafasi hiyo katika kura za maoni za chama hicho.

Hivi karibuni Mbunge wa Ilala Mussa Zungu, alikariliwa na vyombo vya habari akisema kwamba hatishwi na baadhi wanachama wenzake wanaoutaka ubunge katika jimbo hilo kupitia kwenye mitandao ya kijamii kama vile Fecebook.

No comments:

Post a Comment