KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday 16 August 2015

BENKI YA CRDB YAZINDUA HUDUMA ZA MALIPO KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI HOSPITALI YA RUFAA YA MBEYA

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kulia), akimkabidhi mfano wa kadi ya malipo ya Tembo Card, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini, Myriam Msalale (kushoto),  itakayowawezesha wagonjwa wanaofika katika hospitli hiyo kulipia huduma za matibabu kwa njia ya kadi badala ya fedha taslimu. Uzinduzi huo ulifanyika mjini Mbeya mwishoni mwa wiki. (Na Mpiga Picha Wetu)
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa benki ya CRDB baada ya kuzindua huduma za malipo kwa njia ya kielektroniki katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini mjini Mbeya.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini baada ya kuzindua huduma za malipo kwa kutumia mfumo wa kielektroniki badala ya fedha taslimu katika hospitali hiyo. Wa pili kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini, Myriam Msalale.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akilipia huduma za matibabu kwa njia ya kielektroniki katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini baada ya kuzindua huduma hizo. Wanaoshuhudia kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Benki ya CRDB tawi la Mbeya, Benson Mwakyusa,  Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini, Myriam Msalale na  Rahel Massawe.
Mkurugenzi wa Benki ya CRDB tawi la Mbeya, Benson Mwakyusa (wa pili kulia) akiangalia risiti ya malipo baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei kulipia huduma za matibabu kwa njia ya kielektroniki wakati wa uzinduzi wa huduma hizo katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini, mjini Mbeya, mwishoni mwa wiki.
  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini, Myriam Msalale akimtembeza katika vitengo mbalimbali vya hospitali hiyo,  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei.
 Baadhi ya Mameneja wa Matawi ya Benki ya CRDB kutoka mkoani Mbeya wakiwa katika uzinduzi huo. Kulia ni Meneja wa tawi la Mbalizi, Chibby Chibby.
 Mkurugenzi wa Benki ya CRDB tawi la Mbeya, Benson Mwakyusa akizungumza katika uzinduzi huo.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Hospitari ya Rufaa ya Mbeya pamoja na wafanyakazi wa Benki ya CRDB wakiwa katika uzinduzi huo.
 Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB, Godwin Semunyu akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma za malipo kwa njia Kielektroni katika hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Huduma Mbadala za Benki wa CRDB, Joseph Witts, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini, Myriam Msalale.
  
Na Mwandishi Wetu, Mbeya
UONGOZI wa Hospital ya Rufaa ya Mbeya, imeingia makubaliano na benki ya CRDB ambapo sasa wananchi watalipia huduma kupitia mfumo maalum wa kielektroniki kwa kadi za benki hiyo badala ya fedha taslimu.
Akizungumza kwenye hafla fupi ya kuzindua huduma hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa hospitali hiyo, Myriam Msalala, alisema kuwa huduma hiyo itaisaidia hospitali hiyo kuongeza makusanyo ya fedha.
Alisema kuwa awali kabla ya kuanza kutumia  mfumo huo, hospitali hiyo ilikuwa ikikusanya kiasi cha Sh. Milioni 38 kwa mwezi na kwa sasa wanakusanya milioni 50.
“Kwa kweli tunawashukuru sana CRDB, kwa sasa hakuna mianya ya upotevu wa fedha kwa kuwa hatutumii tena mfumo wa malipo ya fedha taslimu, tunakusanya kupitia kadi za benki,” alisema Myriam.
Alisema kuwa hakuna mwananchi ambaye atakubaliwa kulipia kwa fedha taslimu na badala yake wanapewa elimu ya kutumia mfumo huo wa kadi za benki.
“Wagonjwa wanaokuja hapa, watakuwa na kadi za benki ambapo baada ya kupatiwa huduma watatoa kadi kw wahuduma wetu au wakala na tutakata malipo hayo,” aliongeza kusema Myriam.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa CRDB, Dk Charles Kimei, alisema kuwa benki hiyo tayari imeingia makubaliano na hospitali zaidi ya 20 ikiwemo Hospitali ya taifa ya Muhimbil kwa ajili ya huduma hiyo.
“Huu ni mfumo salama, na tayari tupo kwenye mazungumzo na hospitali nyingine kubwa ili kujiunga katika mfumo huu, kwa sasa tayari hospitali 20 tumekshakubaliana nazo,” alisema Kimei.
Alisema mfumo huo utarahisisha huduma za hospitalini na kupiunguza gharama za uwendeshajiwa hospitali.
Uzinduzi huo wa mfumo mpya wa  malipo ulishuhudiwa na wakurugenzi na wafanyakazi wa CRDB na wafanyakazi wa hospitali hiyo.

No comments:

Post a Comment