Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda |
Alisema hivyo baada ya kubaini barabara zilizojengwa kushindwa kudumu
kwa muda uliotarajiwa na hivyo kuzua malalamiko kutoka kwa watumiaji na walipa
kodi kwa ujumla.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini jana, Makonda, alisema Manispaa
ya Kinondoni ni wilaya yeneye mtandao mkubwa wa barabara za lami kuliko wilaya
zote 166 Tanzania Bara.
“Manispaa ya Kinondoni ina barabara za lami zenye urefu wa kilometa
241.1 ambazo ni sawana asilimia 22 ya barabara za lami katika halmashauri zote
(kilometa 1,117.5),”alisema Makonda.
Alisema, ukiukwaji huo ulijitokeza katika ushahidi wa kuonesha kuwa
makablasha ya zabuni yalithibitishwa na Bodi ya Zabuni, hakukuwa na makadirio
ya kihandisi ya thamani ya kazi.
Aidha, Makonda, alisema katika maeneo mengine haukufanyika usanifu na
pia hakukuwa na michoro ya kihandisi kwa barabara zote.
“Maelezo ya kazi kwenye jedwali la bei hayakuwa na uhusiano na
viwango vya kazi husika,”alisema Makonda.
Makonda alisema baada ya kupokea ripoti hiyo, atakutana na Mkurugenzi
wa Manispaa hiyo ili kuona ni hatua gani zitakazochukuliwa kwa watendaji wote
waliohusika katika ujenzi wa barabara hizo kwa kiwango cha chini.
“Watakaobainika katika ubadhilifu huo itabidi wafukuzwe kazi kazi na
kama atashindwa kuwafukuza basi kunaulazima wa kufanyakazi kwa waliowateua
wahusika,”alisema Makonda.
No comments:
Post a Comment