KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday 7 August 2015

WAKALA WA FORODHA (TAFFA), 500 NCHINI KUGOMA

ZAIDI yawanachama 500 wa Wakala Forodha (TAFFA), wamesema watagoma kutoa huduma nchi nzima endapo serikali itashindwa kuondoa dhamana ya sh. milioni 100 ambazo ni kwa ajili ya kuhuisha leseni za uwakala wa forodha mwaka 2016.
 Mgomo huo unatarajiwa kufanyika baada ya kupita siku saba walizoipa serikali, ambazo zimeananza jana.
 Walisema hivyo baada ya kubaini njama za TRA kwa kushirikiana na baadhi ya kampuni kubwa kwa lengo la  kutaka  kuzifuta kampuni za wanyonge  ili kampuni kubwa na za kigeni ziweze kunufaika na biashara hiyo.
 Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Rais wa Wakala (TAFFA), Stephen Ngatunga, alisema walishtushwa na tangazo liliotoka
Kwenye gazeti la serikali Julai 22 mwaka huu linawanyima uhuru katika soko la ushindani la Afrika Mashariki.
“Madhara yatakayotokana na amri ya TRA yakuweka sh. milioni 100; ni kampuni nyingi za kitanzania zitakufa, familia nyingi Tanzania nzima zitaumia kutokana na ajira zao kupotea na itajengeka chuki kati wananchi na serikali,”alisema Ngatunga.
Alisema nia ya kukutana na serikali kuu kutaka kusikilizwa kilio chao kuhusu dhamana hiyo, kwani kuna upungufu mwingi unaotekelezwa na TRA ambao wataifahamisha serikali katika kikao hicho wanachoomba.
Ngatunga, alisema tangu kuanza jambo hilo Novemba mwaka jana wamefanya jitihada za kuonana na Waziri wa Fedha na Uchumi Saada Salumu Mkuya lakini bila mafanikio.
Alisema miongoni mwa majibu waliyopewa na TRA kwa mdomo: Biashara ni mchezo kama michezo mingine, anayeweza kucheza acheze, asiyeweza mchezo, mchezo utakuwa umemshinda.
“Tunaiagiza Wizara ya Fedha na Uchumi kuondoa agizo lao la kuweka sh. milioni 100 mara moja, ili kuweza kuimarisha umoja na mshikamano wa kitaifa na kuiagiza TRA kuondoa fikra za kibaguzi kwa Watanzania.
 “Haya yote yanatokana na maamuzi yaliyotokana na vikao vilivyoketi Zanzibar na Azimio la Zanzibar ambalo linaelekekeza kaba ikishindikana kufikiwa hatua ya mazungumzo basi wasitishe huduma nchi nzima ,”alisema Ngatunga.
 Naye Rais ZFB, Omar Hussein Mussa, alisema anaamini kuwa hatua hiyo ya kugoma itafuatia baada ya kushindikana mazungumzo, ambapo anaamini kila kitu kinawezekana watakapokutana mezani na serikali.












No comments:

Post a Comment