KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Monday 18 January 2016

DIWANI ATAKA HAKI ITENDEKE BOMOABOA KIMARA


DIWANI  wa Kata ya  Saranga Kimara jijini  Dar es Salaam ,  Ephraim Kinyafu, amesema hadi sasa  Shirika la Maji Safi na Majitaka (Dawasa),imeweka alama ya ‘X’nyumba 15 Matangini, nyumba 50 Stop Over na bado wanaendelea kuweka alama nyumba nyingine kwa ajili ya ubomoaji.

Kauli ya Kinyafu imekuja siku moja baada ya wananchi wa Kimara Matangini kulalamikia kitendo cha Shirika la majisafi  na  majitaka(Dawasa) kuwataka wabomoe nyumba zao kwa madai kuwa wamejenga juu ya bomba la maji na wasipofanya hivyo ikiwabomolea  watalipa gharama.

Akizungumza  na jijini leo, Kinyafu  alisema nyumba hizo zimebainika kuwa zimejengwa kimakosa lakini pia ameshangazwa na nyumba nyingine ambazo zimewekewa  alama ya ‘X’  ambazo  zipo  umbali wa mita 7.5 toka katikati ya bomba hilo.

“Upimaji wa upana halisi haujazingatiwa kuna maeneo wamepima zaidi ya mita tano,mita 9 mpaka 14”.alisema Kinyafu.

Alisema sheria ya mwaka 1964 inasema upana halisi toka bomba hilo inatakiwa kuwa mita tano lakini anashangaa Dawasa walishaweka alama katika nyumba nyingine ambazo zipo nje ya mita tano nyumba hizo  zipo umbali wa  mita 7.5, mita 9 na nyingine mita 14.

Kinyafu alisema tangu wananchi hao wapewe amri ya kubomoa, wananchi zaidi ya 30 hawana makazi ya kuishi.

“Kuna mwanamke mmoja ambaye jina lake silifahamu anawatoto saba na wajukuu hana mahali pa kuishi na hivi sasa amehifadhiwa na jirani”alisema Kinyafu.

Kinyafu  alisema ameongea na Dawasa wakishirikiana na Dawasco waongeze muda ili wananchi wapate nafasi ya kuhamisha mali zao na sio kutaka  wavunje haraka kwani watapata athari kwa kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment