CHAMA cha Wapangaji Tanzania (TTA), kinatarajia kutakutana na Waziri
wa Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, January Makamba hivi karibuni,
kuzungumzia hatima ya mali
za wapangaji waliyokumbwa na bomoaboa katika nyumba zilizokuwa mabondeni.
Ripoti ya Serikali inaonesha kuwa hadi sasa nyumba za wakazi
774 zimebomolewa, ambapo ni wakazi 20 tu ndiyo walikuwa na hati halali
za makazi huku 119 wakiwa na leseni za makazi za muda mfupi.
Katibu Mwenezi wa TTA, Simon Kwezi, aliyasema hayo baada ya chama
hicho kubaini kuwa serikali imeonesha kutoguswa na mahangaiko waliyoyapata
wapangaji ambao ndiyo waliyokuwa wakiishi katika nyumba hizo na baadala yake
imeamua kuwalipa fidia baadhi ya wamiliki wa nyumba hizo.
Alisema, kabla ya kukutana na waziri huyo, chama hicho kimewataka
wapangaji wote waliyokuwa wanaishi katika nyumba zilizokumbwa na bomoabomoa
kujitokeza katika ofisi za chama hicho, kwa ajili ya kujiorodhesha kisha idadi yao akabidhiwe waziri
huyo ili ikiwezekana serikali iwafidie.
Kwezi, alisema ili kupata orodha halali ya wapangaji hao, TTA
imejipanga kufanya shughuli hiyo kwa kushirikiana na wenyeviti wa Serikali za
Mitaa na wajumbe wakekatika maeneo yote ya jiji yaliyokumbwa na bomoabomoa
hiyo.
“Tunaiomba serikali iwafidie wapangaji hawa kwani hawa ndiyo
waliyoathirika zaidi katika bomoabomoa hiyo ukilinganisha na wa miliki kwani
wao hawakuwa wakiishi katika nyumba hizo kutokana na kujua athari za kuishi
maeneo hayo tangu awali.
“Tunajipanga kukutana na waziri ili kuona ni jinsi gani ya kuwasaidia
wapangaji na endapo itashindikana kupatikama muafaka itawalazimu kwenda
mahakamani kudai haki hiyo ambayo ni fidia,”alisema Kwezi.
Akizungumzia mikataba ya upangaji, alisema kuwa wapangaji wasikubali
kuingia kwenye nyumba bila ya mkataba unaotambulika kisheria.
Alisema kitendo cha kuingia kwenye nyumba bila ya mkataba
unaotambulika kisheria kimekuwa chanzo cha wamiliki hao kuongeza kodi mara kwa
mara kwa wapangaji kutokana na tamaa binafsi ambazo zinasukumwa na uroho wa
kipato.
“Tunawashauri kila wanapotaka kupanga wafike kwenye ofisi zetu popote
katika maeneo husika ili waweze kupatiwa msaada wa kisheria kwa chama chetu
kinao wanasheria kwa ajili ya kupigania haki zenu,”alisema.
Kuhusu Madalali, Kwezi, alisema genge hilo limekuwa kikwazo kikubwa katika kupanda
bei za upangaji wa myumba mijini.
“Hawa ni watu hatari kwani wamekuwa wakitumia ujanja wa kula kwa
mpangaji na wamiliki, kwa hiyo ili kuepuka hayo ni vema wamiliki wakasajili
nyumba zao katika ofisi za TTA ili kiweze kusimamia haki,”alisema.
Ili kukomesha
magenge ya watu wachache wanaojiita madalali huku wakiwa hawana usajili wala
hawalipi kodi serikalini, Kwesi alisema umefika wakati kwa serikali kuunda
chombo kitakachopambana na magenge hayo ambayo huamua kuwalipisha wapangaji
kodi ya kipindi cha miezi mitatu au mwaka jambo ambalo kisheria halikubaliki.
No comments:
Post a Comment