KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday 14 February 2016

 TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII AFRIKA MASHARIKI NA KATI (ECASSA)

 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Tanzania, (TSSA), Meshack Bandawe, (katikati), akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam, Februari 14, 2016. Pamoja na mambo mengine Bandawqe alisema, mkutano wa mwaka wa Muungano wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na Mamlaka za Usimamizi Sekta za Hifadhi za Jamii kwa Nchi za Afrika Mashariki na Kati (ECASSA), utafanyika nchini kuanzia Februari 18mwaka huu 2016. (Kushoto) ni Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo, Vincent Tiganya, na kulia ni mjumbe wa kamati ya waandaaji wa mkutano, Rehema Kabongo.
…………………………………………………………………………………………………………

MAKAMU wa Rais  Samia Suluhu Hassani anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Mkutano wa muungano wa mifuko ya hifadhi ya jamii(Pensheni na afya), mamlaka ya usimamizi za hifadhi ya jamii za nchi za Afrika mashariki na kati (ECASSA).
Nchi wanachama watakaoshiriki katika mkutano huo ni Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Tanzania, Zambia na Sudani ya Kusini.
Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam leo, Katibu wa Umoja wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Tanzania(TSSA), Meshack Bandawe alisema , dhumuni la mkutano huo ni kujadili sera zinazohusiana na sekta ya jamii.
Alisema mkutano huo utafanyika Februali 18-19 mwaka huu katika ukumbi wa Benki kuu(BOT) ambapo siku ya kwanza washiriki watapokea mada mbalimbali za kitaalamu kuzijadili na kutoa mapendekezo yao.
“Siku ya pili itakuwa maalumu kwa mawaziri kuzungumzia hatua zinazochukuliwa nan chi zao ku[punguza tatizo la ajira. Inapendekezwa kwa upande wa Tanzania itolewe na waziri mmoja kuonyesha hatua za kisera na mipango zinazochukuliwa kukuza ajira na kuboresha hifadhi ya jamii ili kuchangia upunguzaji wa hifadhi.
Alisema mkutano huo pia utapokea mada zilizowasilishwa na wataalamu ambapo zitachambuliwa na kuweka maadhimio kwa ajili ya kuboresha sekta ya hifadhi ya jamii katika nchi wanachama.
“Kwa mara ya kwanza mkutano kama huu ulifanyika mjini mwanza mwaka 2010 na mwaka huu Tanzania inakuwa mwenyeji katika mkutano huo,”alisema.
Alisema kauli mbiu ya mkutano huo ni ‘kuainisha sera za kiuchumi, upatikanaji wa ajira na maendeleo ya sekta ya  hifadhi ya jamii katika Afrika Mashariki na kati’.
Aidha alisema washiriki wa mkutano huo watakuwa Mawaziri wa sekta zenye dhamana katika mifuko ya hifadhi ya jamii(Pensheni, bima ya afya na fidia kwa wafanyakazi).
“Pamoja na  mawaziri hao watakuwepo makatibu wakuu wa Wizara na wajumbe wa bodi za mifuko mifuko hiyo,”alisema.
Muungano wa mifuko ya hifadhi ya jamii Pensheni na afya na mamlaka za usimamizi za hifadhi za  jamii za nchi za afrika mashariki na kati hadi sasa taasisi 23 zinazounda umoja huo.

No comments:

Post a Comment