KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Saturday 14 May 2016

DIWANI WA CHADEMA KATA YA MAKANGARAWE: WAFANYABIASHARA IMARISHENI SOKO LENU



WAFANYABIASHARA wa Soko la Yombo Makangarawe  wamesema kuwa wamejipanga kuliboresha Soko lao huku wakiwataka viongozi wa Kata hiyo kuhakikisha wanashawishi madalali kuleta magari ya bidhaa Sokoni hapo Kwa ajili ya kumwaga kama ilivyo katika masoko ya Temeke Stereo.
Walisema hayobaada ya kukamilika ujenzi wa Soko hilo ambapo kwa muda mrefu kulikuwa hakuna Soko hivyo ujio wa Soko hilo ambalo lilifunguliwa hivi karibuni na kiongozi wa mbio za Mwenge mwaka 2015 kumefanya watu wa  Makangarawe kuwa na Soko lao.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana,  kwaniaba ya wananchi wake Diwani wa Makangarawe  (Chadema), Dk. Idd  Mahuta alisema kuwa mbali na kuwepo kwa Soko hilo bado uendeshaji wake umekuwa  mgumu kutokana na wanchi kukimbilia masoko ya mbali na kuliacha Soko hilo likikosa wateja.
“Kitokana na matatizo hayo tumeamua kuhamasisha wafanyabiashara hao kila aliyepewa kizimba kuhakikisha anafanya biashara hapa,”alisema Mahuta.
Alisema, kuwa matatizo makubwa katika soko hilo ni kwamba watu walikamata vizimba lakini cha kushangaza hawafanyi  biashara sasa ni wakati muafaka  kwa kila mfanyabiashara anaendelezaji  sehemu yake.
"Tunawataka wafanyabiashara wetu kufanya biashara hapa na sisi kama viongozi tutaendelea kufanya jitihada za kuhamasisha watu kuja katika Soko hili kwani eneo linauwezo wa kubeba wafanyabiashara 800 hadi 900,”alisema Dk. Mahuta
Aidha akizungumzia uwezo wa soko hilo Dk. Mahuta, alisema lina uwezo wa kulisha katika maeneo ya Buza hadi Yombo kilakala hivyo kuna haja ya kuliboresha soko hilo ili liweze kukidhi haja.
Pia aliwataka wananchi wote wanaozunguka eneo hilo kuhakikisha wanalitumia Soko hilo ipasavyo kwa ajili ya kuboresha vipato vyao na kipato cha Halmashauri ya Temeke.
Kwaupande wake Mwenyekiti wa Serikali ya Dovyo, Bruce Mbagwile, alisema kata hiyo inamitaa mitano ambapo kimsingi mitaa yote hiyo  inategemea Soko hilo
Aidha, alisema kuwa walichokifanya wananchi hao ni kurudisha muamko kwa wafanyabiashara hao ili kila mmoja aliyechukua kizimba anafanya biashara na si vinginevyo.
Mwisho

No comments:

Post a Comment